• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 3 November 2016

    SERIKALI YATENGA BILIONI 13 KUWEKA MAJI SAFI RUVUMA.



    Serikali
    imetenga jumla ya shilingi bilioni 13.17 katika Bajeti ya mwaka 2016/2017 kwa
    lengo la kutekeleza miradi ya maji katika vijiji vya mkoa wa Ruvuma ili

    kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo wanapata maji safi na salama.
     
    Kiasi
    hicho cha fedha kimetajwa leo mjini Dodoma na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi
    Gerson Lwenge alipokuwa akijibu swali la Mhe. Jacqueline Ngonyani (Viti Maalum)
    lililohoji juu ya muda ambao Serikali itapeleka majisafi na salama katika Mkoa
    Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi
    Gerson Lwenge  akijibu swali Bungeni leo mjini Dodoma.

    huo.
     
    Waziri
    amesema kuwa Mpango wa Utekelezaji wa Maji Vijijini ulioanza mwaka 2006/ 2007, mkoa
    wa Ruvuma ulipangiwa vijiji 80 na kati ya vijiji hivyo jumla ya vijiji 76
    vilipata maji safi na salama.  
     
    “Asilimia
    kubwa ya vijiji vilivyokuwa katika miradi hiyo vimepata maji safi na miradi
    iliyobakia ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji hivyo kwa mwaka huu wa
    fedha Ruvuma imetengewa kiasi cha fedha cha bilioni 13.17 ili changamoto ya
    maji safi na salama katika mkoa huo iishe kabisa”, alisema Lwenge.
     
    Ameongeza
    kuwa Serikali imeendelea na mipango ya kuboresha huduma hizo katika miji ya
    Songea, Mbinga, Namtumbo na Tunduru iliyopo katika mkoa huo ambapo kwa mji wa
    Songea, mradi wa ukarabati wa chanzo cha maji cha mto Ruhila Darajani umekamilika
    kwa gharama ya shilingi bilioni 2.6.
     
    Amefafanua
    kuwa kukamilika kwa chanzo hicho mnamo mwezi Februari mwaka huu kumeongeza
    kiasi cha upatikanaji wa maji wa jumla ya lita milioni 6 kwa siku ambapo wakazi
    164,162 wamenufaika katika Manispaa hiyo.
     
    Aidha,
    Mhandisi Lwenge amebainisha kuwa kwa sasa Serikali imekamilisha usanifu wa kina
    na uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya uboreshaji wa huduma hizo katika
    miji iliyopo katika mkoa huo.
     
    “Serikali
    inaendelea na jitihada ya kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi
    hiyo ambayo kwa mji wa Tunduru mradi utagharimu
    Dola za Kimarekani milioni 7.3, mji wa Namtumbo ni Dola za Kimarekani
    12.08, na Dola za Kimarekani 11.86 kwa ajili ya mji wa Mbinga”, alisema
    Mhandisi Lwenge.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI