Habari
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amenusa ufisadi katika mradi wa ujenzi wa nyumba za Avic “Avic Town’ na kuitaka taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru), kuuchunguza mradi huo uliopo Kigamboni jijini humo.
Hatua hiyo imefika baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi waliokuwa wakiishi eneo hilo na kutolewa pasipo kupewa fidia zao huku ekari 18 za Chama cha Mapinduzi (CCM),zikichukuliwa kwa matumizi katika mradi huo.
Akizungumzia hatua hiyo, Makonda alisemakuwa leo watendaji wa serikali wanaohusika na taarifa za mradi huo kumfikishia taarifa sahihi kwani hataki kuona ubadhilifu na kuona haki inatendeka kwa wananchi hao.
“Sitaki kuona kigogo wala kijiti anahusika katika mradi huo, Nitasimamia na polisi waliohusika katika kuwatoa wananchi hawa waseme walitumia vigezo gani kuwatoa,”alisema.
Alisema wananchi walioondolewa eneo hilo wafike kwa Mkuu wao wa Wilaya huku Takukuru wakipaswa kufanya kazi yao ili wananchi wapate haki zao.
Akizungumza huku akilia mkazi wa eneo hilo ambaye pia ni mwathirika wa mradi huo, Pascalina Walioba alisema tangu mradi utambulishwe na kuanza kujengwa hawajalipwa stahiki zao.
“Mimi ni mwathirika wa mradi huo, tangu unaanzishwa na tukahamishwa …kipindi hicho nilipaswa kulipwa Sh 700,000 lakini hadi leo sijalipwa na thamani ya fedha inaongezeka,”alisema na kisha kuangua kilio.
Mbunge wa Jimbo hilo, Faustine Ndungulile alisema kuwa wapo watu walikuwa wakidai kuwa ujenzi ule unahusisha nyumba za ulinzi wa usalama.
“Kuna hekari 18 za Chama cha Mapinduzi (CCM) zipo humo lakini tutalifualia,”alisisitiza Ndungulile.
Katika hatua nyingine Wilaya hiyo imeahidiwa na Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco), hadi kufikia February mwakani watakuwana umeme wa uhakika.
Aidha wananchi wa eneo hilo walitolewa hofu juu ya upatikanaji wa maji safi kwani tayari maji yapo ya visima lakini hakuna mabomba ya kusafirisha maji hayo.
Akizungumzia mradi wa maji katika mji huo, Mwakilishi kutoka Shirika la Maji saifi na Maji taka(Dawasco),….alisema fedha zilizotengwa katika kusambaza maji katika wilaya hiyo ni Sh bilioni 40 huku fedha zinazoitajika ili kukamilisha mradi huo ni Sh bilioni 146.
“Najua mnahitaji maji safi na salama na sisi tunapambana ili mpate maji ya uhakika tunakuomba Mkuu wa Mkoa utufikishie kilio chetu kwa rais ili bajeti inayotengwa kwa ajili ya maji iongezwe,”alisema.
Jiunge nasi
No comments:
Post a Comment