• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday 31 December 2016

    SALAMU ZA DC MJEMA KUHUSU KIPINDUPINDU NA SHEREHE ZA MWAKA MPYA KWA WANAVINGUNGUTI

    dc-mjema-usafi-dec-31-2016-57Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amewataka wakazi wa Mtaa wa Kombo Kata ya Vingunguti kutunza mazingira yao kwa kufanya usafi mara kwa mara ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu kwani imekuwa ikiripotiwa mara kwa mara kuwa wagonjwa wengi wa kipindupindu wanatokea maeneo hayo.dc-mjema-usafi-dec-31-2016-57

    DC Mjema ameyasema hayo alipokuwa akihamasisha suala la kufanya usafi kwa vitendo ikiwa ni agizo la Rais Magufuli kwa watanzania kufanya usafi kila Jumamosi ya kila mwisho mwezi ambapo amewasisitizia kuwa suala la usafi nila kila mmoja hivyo wajitokeze kufanya usafi kwa hiari yao bila kulazimishwa kwa ilivyokuwa hapo awali.dc-mjema-usafi-dec-31-2016-54

    Katika hatua nyingine DC Mjema amewataka wakazi hao kusherekea sikukuu ya mwaka mpya kwa amani bila kuchoma matairi wakiwa majumbani mwao, kwani kutakuwa na oparesheni maalum kwa watakaofanya vitendo vya uvunjifu wa amani.dc-mjema-usafi-dec-31-2016-51

    Kwa upande wake Naibu Meya na Diwani wa Kata hiyo Omary Kumbilamoto amewataka wakazi hao kuendelea kujitokeza kwenye usafi kama walivyofanya leo mbele ya DC Mjema kwani ni kwa faida yao wenyewe, pia Naibu Meya huyo amemkabidhi DC Mjema mbuzi kwa ajili ya kusherekea sikukuu ya mwaka mpaya wa 2017 na kuunga mkono jitihada zake za kuleta maendeleo katika wilaya ya Ilala.dc-mjema-usafi-dec-31-2016-56dc-mjema-usafi-dec-31-2016-58dc-mjema-usafi-dec-31-2016-55dc-mjema-usafi-dec-31-2016-46

    Jiunge nasi 

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI