kuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amefanya ufunguzi wa jengo la Upasuaji kwa wanawake wajawazito
katika Hospitali ya Mwananyamala Wilaya ya Kinondoni jengo lilidhaminiwa na Taasi ya GSM Foundation, ambapo jengo
hilo limepewa jina la Makonda Obstetric Theatre kutokana na yeye kuwa muasisi wa jitihada hizo za ujenzi alipokuwa
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kabla ya kuteuliwa na Rais John Pombe Magufuli March 13 Mwaka jana kuwa Mkuu wa Mkoa
Akizungumzia ujenzi wa jengo hilo RC Makonda amewapongeza GSM Foundation na kuwataka watanzania waunge mkono
jitihada za wawekezaji wanao wekeza ndani ya nchi na kuwataka wananchi kununua bidhaa za wazawa kwani mwisho wa siku wanairejesha
faida kwa wananchi kwa kufanya miradi ya maendeleo kama hiyo, huku akisisitiza suala la ulipaji kodi kwa kila mtanzania serikali yeyote duniani haiwezi
kujiendesha bila ya kulipa kodi ndiyo maana Rais Magufuli anasisitiza kulipa kodi, hivyo kila mtanzania ajue anamchango katika maendeleo ya taifa kwa kulipa kodi .
Akitoa Muhtasari waMradi Mhandisi kutoka Taasisi isiyo ya kiserikali ya GSM Foundation waliodhamini ujenzi huo Hersi Saidi
ameeleza kuwa ujenzi huo umegharimu kiasi cha shilingi Milioni 420 na kuna vyumba viwili vya upasuaji,
huku akisisitiza kuwa watanzania wawe na moyo wa kujitolea kama walivyofanya wao.
Kwa upande wake Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sitta
ameeleza kuwa jengo hilo ni muhimu sana kwani linauwezo wa kuhudumi kinamama kati ya 40 na 50 kwa siku hivyo
kati ya wanawake 20 na 30 ufanyiwa upasuaji na kupelekea kuondoa msongamano uliokuwepo awali
na kufanya huduma zichelewa, pia utaokoa maisha ya wanawake.
No comments:
Post a Comment