Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam mh Paul Makonda amewataka wana nchi wa Mkoa wa Dar es salaam, kujitokeza kwa wingi kesho katika ufunguzi rasmi wa sehemu ya kwanza ya mradi wa mabasi ya mwendo wa haraka /mwendo kasi DART , utakao fanywa kesho na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe.
Dr John P Magufuli kesho January 25.
Amesema uzinduzi huo utakuwa ni mwendelezo wa jitihada kubwa zinazo fanywa na serikali katika kutatua kero mbalimbali za wananchi hasa katika kupunguza msongamano barabarani hapa mjini.
Mradi wa usafiri wa mabasi ya mwendo kazi ulianza kutumika kwa kibali maalumu cha Rais Magufuli tangu tarehe10/5/2016 kwa safari za kumara ,kivukoni ,morocco ambazo zinahusisha jumla ya kilomita 20.9 Ikiwa ni sehemu ya kwanza ya mradi huu
Ufunguzi huo utafanyika kuanzia saa 8:00 asubuhi katika kituo cha DART Gerezani kariakoo
No comments:
Post a Comment