• Breaking News

    ..

    ..

    Sunday, 19 February 2017

    OPERESHENI LIPA KODI YA PANGO LA ARDHI”


    2
    Mhe. Mabula akikagua mifumo ya ulipaji kodi ya pango la Ardhi sambamba na kuhakiki kumbukumbu za umiliki wa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza.
    Ikiwa Operesheni Lipa Kodi ya Pango la Ardhi inaendelea, ambapo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea kutoa notisi ya siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Kodi ya pango la Ardhi huku ikiendelea na kuhabarisha Umma kuhusu umuhimu wa kuzingatia Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999, katika vifungu Na. 49 na 51 ambavyo vinadhihirisha ruhusa ya mmiliki kufutiwa umiliki wa ardhi kama mmiliki hatazingatia kulipa Kodi ya Pango la Ardhi.
    Kwa upande wake; Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelea ya Makazi, Dkt Angeline Mabula (Mb), amekuwa akifanya ziara ya kukagua mifumo ya ulipaji kodi ya pango la Ardhi sehemu mbalimbali nchini.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI