• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 16 February 2017

    Watanzania watakiwa kubadilisha kadi mpya za Homa ya Manjano

    Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa taratibu mpya za utoaji wa chanjo ya Homa ya Manjano (Yellow Fever) kupitia vituo vilivyoidhinishwa hapa nchini.
    Akizungumza na waandishi wa Habari mapema leo 16 Februari 2017, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Afya, Mh. Ummy Mwalimu  amebainisha kuwa kila msafiri atatakiwa kupata chanjo halali na kupewa cheti maalumu cha chanjo ya Homa ya Manjano yaani ‘International Certificate of Vaccination’ kama utambulisho kwamba amepata chanjo ya Homa ya Manjano.
    “Wizara imefanya maboresho ya vyeti vya chanjo ya Homa ya Manjano ambavyo nilivizindua tarehe 24/11/2016. Lengo likiwa ni kudhibiti utolewaji holela wa vyeti hivi.  Vyeti hivi vipya vilianza kutolewa kuanzia tarehe 1 Agoslinaendelea kutolewa katika vituo vya Afya vya Serikali vilivyo idhinishwa hadi sasa” ameeleza Waziri Ummy Mwalimu.
    Waziri Ummy Mwalimu pia ameongeza kuwa, Wananchi wote wenye vyeti vya chanjo ya Homa ya Manjano  vya zamani ambao walipatiwa chanjo na kupewa vyeti halali kuwa, wawasilishe vyeti hivyo na hati ya kusafiri kwenye kituo cha Afya alichopatiwa cheti ambako kumbukumbu za chanjo zipo ili aweze kupatiwa cheti kipya. Gti, 2016 zoezi  likienda kwa gharama ya Tsh. 5000  na kwa raia wa Kigeni ni Dola 10 pekee.
    Chanjo hiyo hutolewa kwa wasafiri wanakwenda kwenye nchi 30 za Bara la Afrika  ambazo ni Angola, Benin, Burkina Faso, Burundi, Cameron, Afrika ya Kati, Chad, Congo,   Ivory Coast, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Equatorial Guinea, Ethiopia, Gabon, Gambia, Ghana, Guinea, Ginea Bissau, Kenya, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Nigeria, Rwanda, Senegal, Sierra Leone,  Sudan ya Kusini,  Sudan, Togo, Uganda.
    Pia kwa nchi 13 kutoka Bara la Amerika ya Kusini ambazo ni  Argentina, Bolivia, Brazil, Colombia, Ecuador, French Guiana, Guyana, Panama, Paraguay, Peru, Suriname, Trinidad, Venezuela kama  zilivyoainishwa na WHO kuwa na hatari ya maambukizi ya ugonjwa wa Homa ya Manjano Wasafiri wanaokwenda nchi hizi wahakikishe wanachanja chanjo ya Homa ya Manjano siku 10 kabla ya kusafiri na kisha kupewa cheti cha kuthibitisha kupata chanjo hiyo.

    Mkutano huo ukiendelea
    Katika hatua nyingine, Waziri Ummy Mwalimu amekitupia lawama kituo cha Mnazi Mmoja kwa hatua yake ya kutoa vyeti vya Chanjo bila kuchanjwa.
    “Ni  wajibu wa kila msafiri nchini kuepuka kupokea au kununua vyeti vya chanjo ya manjano bila kupata chanjo kwani kufanya hivyo sio tu ni kosa la jinai bali pia kunahatarisha maisha ya msafiri na ya watu wengine. Aidha, ninawaomba wananchi kutoa  taarifa kwenye ofisi yoyote ya Serikali iliyo karibu au vyombo vya dola endapo watabaini  Afisa au mtu anatoa cheti cha njano bila chanjo hiyo kutolewa.
    Kitendo hiki ni kinyume na Sheria ya Afya Jamii ya Mwaka, 2009. Hatua kali zitachukuliwa kwa mtu yeyote anayetengeneza, kuuza au kununua vyeti visivyo halali vya chanjo” alieleza Ummy.
    Ameongezea kuwa, Zoezi hilo la kubadilisha vyeti vya zamani  vya chanjo ya manjano limeanza tangu  tarehe 09 Januari, 2017  na litadumu hadi tarehe 31   Machi, 2017. Kuanzia tarehe 01 Aprili, 2017 vyeti vya zamani vya chanjo havitatambulika tena hivyo wananchi wote wenye vyeti halali vya zamani wawasilishe vyeti hivyo kwenye vituo vya Afya walikopatiwa Chanjo ya Homa ya Manjano ili vibadilishwe.
    Vituo hivyo  ni pamoja na Viwanja vya Ndege wa Kimaitaifa wa Julius Nyerere, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro na Uwanja wa Ndege wa Mwanza. Pia katika bandari ya Dar es Salaam, Bandari ya Tanga, Bandari ya Mwanza na Bandari ya Kigoma.
    Katika mipaka ya nchi kavu ni pamoja na Horohoro, Namanga, Holili, Tarakea, Sirari, Isaka, Mutukula, Mtambaswala, Kasumulu na Tunduma. Huku kwa Jiji la Dar es Salaam,  ni pamoja na kituo cha Mnazi Mmoja.

    Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) mapema leo wakati wa kuzungumzia suala hilo la vyeti vipya vya homa ya Manjano. Anayefuatia ni  Mkurugenzi wa Uhakiki na Ubora wa Huduma za Afya Dk. Mohammed Mohammed

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI