
Malaysia imesema kuwa itasalimisha mwili wa ndugu wa kambo ya kiongozi wa Korea Kaskazini aliyeuawa kwenda Korea Kaskazini.
Waziri mkuu Najib Razak, anasema kuwa serikali ilikuwa imeidhindsha kusalamishwa mwili wa Kim Jong-nam.Bwana kim aliuawa kwenye uwanja wa ndege Kuala Lumpur na kemikali kali mwezi uliopita.
- Je nani ni muuaji wa Kim Jong Nam?
- Korea Kaskazini ndiyo ilimuua Kim Jong-nam, yadai Korea Kusini
- Mshukiwa wa mauaji ya Kim Jong nam akamatwa
Waziri mkuu Najib anasema kuwa raia 9 wa Malaysia ambao wamekuwa wakizuiwa kuondoka Korea Kaskazini, sasa wamepewa ruhusa wa kuondoka nayo Malaysia itawaruhusu raia wa Korea Kaskazizi kuondoka.

Wachunguzi wa Malaysia walikuwa wameitaka Korea Kaskazini kusalimisha washukiwa watatu kati yao wakiwa kujificha kwenye ubalozi wa Korea Kaskazini nchini Malaysia.
- Malaysia yawafukuza watu 50 raia wa Korea Kaskazini
- Wafanyakazi wa UN raia wa Malaysia waliozuiliwa Korea Kaskazini waondoka
Wanawake wawili mmoja raia wa Vietnam na mwingine raia wa Indonesia wamekamatwa kwa mauaji ya Kim.
Wote wanasema walifikiri walikuwa wakiigiza katika mchezo wa televisheni
No comments:
Post a Comment