• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 30 March 2017

    MKUU WA WILAYA YA ILALA AMEZINDUA WI-FI CHUO CHA CBE JIJINI DAR ES SALAAM

    Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema amezindua WiFi ya mtandao wa  bure kwa katika chuo cha elimu ya biashara (CBE) kampasi ya Dar es Salaam, na kuwaomba wanafunzi wa chuo hicho kuitumia WiFi hiyo kwa tija ya masomo ikiwemo kufanya tafiti mbalimbali zitakazo wasaidia katika masomo yao na jamii kwa ujumla.
     
    DC Mjema ameupongeza mradi huo wa WiFi ya bure ambao unaendeshwa na kampuni ya Tanzanite Technology Co. Ltd kwa kushirikiana na manispaa ya Ilala na kampuni ya simu ya TTCL  kwani unataraji kuwanufaisha zaidi ya watumiaji 7000 ambao ni wahadhili, wafanyakazi, wanachuo na wadau mbalimbali.




    Huku lengo kubwa likiwa ni kujenga daraja la Teknolojia na kuondoa pengo kati ya walio na uwezo wa kutumia mtandao wa Internet na wasio kuwa na uwezo, ambapo DC Mjema amesisitiza endapo kutakuwa na matumizi sahihi ya Teknolojia hiyo taifa kwa ujumla litapiga hatua na ufaulu kuongozeka kwa wanafunzi nchini.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI