Dr Mwakyembe ameyasema hayo Mkoani Dodoma alipohojiwa na muandishi wa habari za michezo, sababu za yeye kuondoka mapema katika mchezo huo kabla kuisha. Baadhi ya viongozi wa soka Mkoani hapo pamoja na wadau wa soka waitupia lawama klabu hiyo kwa kuwapelekea kikosi chapili badala ya kile walicho kitarajia.
katika uwanja huo wa Jamuhuri, kumechezwa michezo miwili hapo jana, ambapo mchezo wa kwanza ulikuwa ni kati ya Wabunge wa bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya baraza ka wawakilishi kutoka zanzibar, mchezo uliomalizika kwa timu ya Bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania wakichomoza na ushindi wa magoli 4 kwa 0.
Mchezo uliofuata ulikuwa ni kati ya timu ya kombaini ya majeshi dhidi ya klabu ya yanga, mchezo uliomalizika kwa kutoshana nguvu ya goli moja kwa moja.
No comments:
Post a Comment