Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam PAUL
MAKONDA, ametoa agizo hilo wakati akizungumzia na wandishi wa habari kuhusu miradi inayototekelezwa Mkoani
humo ikiwemo ya DMDP, huku akisema tayari ameshaiandikia barua TAKUKURU ili
kutekeleza agizo hilo.
MAKONDA alisema, kuwa Wilaya Ilala na
Temeke ndizo zimeongoza kwa kukiuka taratibu na kufanya ubadhilifu wa zaidi ya
shilingi Bilioni-5 na Kinondoni zaidi ya shilingi Bilioni-1.
Kwa upande wa Temeke na Ilala hali
hiyo imebainika baada ya kutaka kujiridhisha na kuweka kumbukumbu sawa kabla ya
kusaini vitabu kwa ajili ya kupitisha fedha za miradi ya DMDP ambapo baada ya
kufanya uchunguzi ikagundulika kwamba vitabu Vinane vimekiuka taratibu na
masharti.
No comments:
Post a Comment