Katibu Mtendaji Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akizungumz ana waandishi
wa Habari (hawapo pichani) juu ya Maonesho ya Mifuko ya Uwezeshaji
wananchi kiuchumi yatakayofanyika katika viwanja vya mashujaa kuanzia
tarehe 18-22 April 2017.
Katibu Mtendaji Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akimskiliza Mhasibu Mkuu
kutoka Mfuko wa Rais wa kujitegemea Bw.Ahazi Kibona juu ya shughuli
mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.
Katibu Mtendaji Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Bi.Beng’I Issa akipata maelezo kutoka
kwa Mkurugenzi Mtendaji kutoka Mfuko wa Pembejeo na Zana za kilimo wa
Taifa Bi.Mariam Nkumbi juu ya shughuli mbalimbali zitokanazo namfuko
huo.
Picha na Daudi Manongi-MAELEZO.
……………………………………………………………….
Na Daudi Manongi-MAELEZO.
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa
atafungua maonesho ya Mifuko ya Uwezeshaji wananchi kiuchumi
yatakayofanyika mkoani Dodoma katika viwanja vya mashujaa kuanzia tarehe
18-22 April 2017.
Akizungumza na waandishi wa
Habari Katibu Mtendaji Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi(NEEC) Bi.Beng’i Issa amesema Maonyesho hayo yameandaliwa na
Baraza hilo kwa lengo la kutoa elimu kwa umma juu ya huduma mbalimbali
zitolewazo na mifuko yote ya uwezeshaji wananchi kiuchumi.
“Tumeamua kufanya maonesho haya
kwa mara ya kwanza kwa sababu changamoto kubwa tuliyonayo ni kuwa mifuko
hii haifahamiki sana na wananchi, wengi walikuwa hawajui wafanye nini
ili waweze kupata fursa ya kupata mitaji na kusaidiwa na mifuko hii
ambayo imeanzishwa na Serikali kwa ajili yao”,Aliongeza Bi.Beng’i.
Amesema maonyesho hayo yatawapa
wananchi fursa ya kuonana na watu ambao wamefanikiwa katika kipindi
kilichopita na hasa kujua jinsi gani watafaidika na mikopo ambayo
inapatikana kupitia mifuko hii.
Ameitaja mifuko ambayo
itashiriki ni pamoja na Mfuko wa kuendeleza wajasiriamali wananchi,
Mfuko wa Uwezeshaji wa Mwananchi, Mfuko wa Pembejeo za Kilimo , Mfuko wa
Maendeleo ya Vijana, Mfuko wa Dhamana za mikopo kwa wajasiriamali
wadogo na wa kati na Mfuko wa Dhamana za Mikopo kwa Mauzo ya Nje ya
Nchi.
Mifuko mingine ni Mfuko wa
kuwasaidia makandarasi,Mfuko wa Maendeleo ya Jamii,Mfuko wa Misitu
Tanzania,SELF Microfinance Fund na PASS Trust Fund.
Kauli mbiu ya Maonyesho haya ni
No comments:
Post a Comment