• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 4 April 2017

    UZINDUZI WA KITUO KIPYA CHA UNUNUZI WA KARAFUU ZSTC PEMBA


    A
    Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo ya kiufundi kutoka kwa Mkurugenzi wa kinga na Elimu ya Afya Dk.Fadhil Mohamed Abdalla  wakati alipotembelea ujenzi wa kituo kipya cha Afya Ngomeni Wilaya ya Cheke Chake Mkoa wa Kusini Pemba leo, akiwa katika ziara maalum ya kikazi.
    A 1
     Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akifungua pazia kuashiria uzinduzi wa Kituo kipya cha ZSTC cha kununulia Karafuu katika kijiji cha Ngomeni Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba,uzinduzi huo umefanyika leo katika ziara maalum ya kikazi katika Mkoa huo.
    A 2
    Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZSTC Dkt.Said Seif Mzee (katikati)mara baada ya kukizindua kituo cha shirika la ZSTC cha ununuzi wa Karafuu katika kijiji cha Ngomeni Wilaya ya Cheke Chake Mkoa wa Kusini Pemba leo, akiwa katika ziara maalum ya kikazi
    A 3
    Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akiangalia  kituo cha shirika la ZSTC cha ununuzi wa Karafuu katika kijiji cha Ngomeni Wilaya ya Cheke Chake Mkoa wa Kusini Pemba leo, akiwa nje mara baada ya kukizindua leo (katikati) Mkurugenzi Mwendeshaji wa ZSTC Dkt.Said Seif Mzee uzinduzi huo umefanyika wakati Rais akiwa katika ziara maalum ya kikazi. 
    A 4
    Maafisa mbali mbali na Wananchi wakiwa katika sherehe za Uzinduzi wa Kituo kipya cha Shirika la ZSTC cha kununulia karafuu katika Kijiji cha Ngomeni Wilaya ya Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba,uzinduzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hatupo pichani),(Picha na Ikulu) 04/04/2017

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI