• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 17 May 2017

    MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU TATU YA POLISI WANAWAKE KUTOKA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA JIJINI DAR ES SALAAM


     Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuluhu
    Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
    Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika
    (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
    Dar es Salaam.
    Muonekaniko wa picha kutoka juu ukionyesha Wajumbe wakati wakimsikiliza  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuluhu
    Hassan kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
    Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika
    (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
    Dar es Salaam.
     Mwakilishi Mkazi wa UN nchini, Alvaro Rodriguez akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
    Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika
    (SARPCO) ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
     Mwaziri wa Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
    Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika
    (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
    Dar es Salaam.
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suuluhu
    Hassan akizungumza na Askari wa Kike wa Kikosi cha Kuzuia Fujo (FFU) mara baada ya kufungua Mafunzo ya siku tatu ya Polisi
    Wanawake kutoka Shirikisho la Majeshi ya Polisi Kusini mwa Afrika
    (SARPCO) kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
    Dar es Salaam.

                            ………………………………………………………………………………….
    Makamu wa
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka
    askari polisi wanawake kutoka kwenye Shirikisho la Majeshi la Polisi Kusini mwa
    Afrika (SARPCCO) washiriki
    kikamilifu katika oparesheni mbalimbali ambazo zinafanyika kwenye ukanda huo kama
    hatua ya kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

    Makamu wa
    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli
    hiyo wakati akifungua mafunzo ya siku Tatu ya Polisi wanawake kutoka nchi
    wanachama wa SARPCCO katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Julius
    Nyerere Jijini Dar es Salaam.

    Makamu wa
    Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewahimiza askari polisi wanawake kufanya kazi
    kwa bidii na kujituma hatua ambayo itasaidia kupanda vyeo kama  askari wanaume katika maeneo yao ya kazi.

    Amesisitiza
    kuwa muda wa kulalamika kuwa hawapandishwi vyeo umeshapitwa na wakati bali kwa
    sasa wachape kazi na waonyeshe kuwa wanaweza majukumu yao wanayopangiwa ili
    waweze kupanda vyeo.

    “Vyeo haviji tu ni
    lazima polisi wanawake muonyeshe kuwa mnaweza ili muweze kupandishwa vyeo na
    kupata nafasi za uongozi katika Majeshi yenu

    Kuhusu utendaji
    kazi wa Polisi wanawake, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amewataka
    polisi hao kutumia mkutano huo wa siku Tatu kujadili kwa kina namna ya kuondoa
    changamoto hizo zinazorudisha nyuma utendaji wao wa kazi.

    Amesema kama
    polisi wanawake wataacha majungu na kujenga umoja na mshikamano miongoni mwao watafikia
    malengo yao haraka hasa katika kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya
    vitendo vya uhalifu ikiwemo biashara ya dawa za kulevya.

    Kwa upande
    wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani Hamad Masauni amesema anaimani kubwa kuwa
    mafunzo hayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa polisi hao wanawake kuimarika
    ipasavyo katika utendaji wao wa kazi.

    Masauni pia
    amewahimiza polisi wanawake wanaopata mafunzo hayo kwenda kuwaelimisha na
    wenzao mipango na mikakati waliyoweka katika kulinda raia na mali zao katika
    nchi zao

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI