• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday, 6 May 2017

    Penzi la mery lauwa nuru yangu

    KAMA UNA MOYO MWEPESI USISOME STORY HII,
    WENGI WAMELIA SANA !!
    “Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu
    aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na
    kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu
    alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari
    kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha
    anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza
    kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili
    ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
    Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu.
    Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake
    aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali
    lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na
    akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule,
    hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa
    kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini
    kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika
    nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha;
    alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia
    kwa Mary. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote
    yalikuwa kwa Mary. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!
    Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa,
    niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke
    wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa
    30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana
    vipande vipande.
    Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana
    mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa
    muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza
    kurudi nyuma kwa sababu Mary aliuteka moyo wangu
    kisawasawa. Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti
    mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia.
    Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.
    Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa
    majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa
    jambo la hakika zaidi.
    Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana
    nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani.
    Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda
    moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara
    moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula
    raha za kufa mtu na Mary
    Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado
    akiandika. Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na
    kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya
    talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu
    lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa
    kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika
    kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye
    tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa
    kadiri itakavyowezekana. Sababu yake ilikuwa ndogo
    lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia
    kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo
    hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya
    kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali
    mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada,
    aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate
    yetu hasa siku ya harusi yetu. Akaniomba na kunisihi
    kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe
    nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa
    kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa.
    Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro
    nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.
    Nilimsimulia Mary kuhusu masharti ya kuachana na
    mke wangu. Mary alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata
    akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’,
    alisema Mary tena kwa dharau. Mimi na mke wangu
    hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya
    kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza
    sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga
    makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama
    mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni
    moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni,
    halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi
    nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema
    kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu
    ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia
    vibaya. Nilimuweka chini nje ya nyumba.
    Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami
    nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili,
    zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani
    pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye
    blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa
    makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua
    hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na
    nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula
    urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini
    namfanyia hivi.
    Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu
    zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na
    tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita
    ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea
    upya. Sikumwambia Mary kuhusu jambo hili. Kadiri
    mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke
    wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya
    kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.
    Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua
    mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna,
    ‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua
    kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo
    maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo
    likanichoma... mke wangu ana uchungu na maumivu
    makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa
    kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema
    ‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’.
    Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo
    la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara
    mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo
    mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo
    katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi
    mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka
    mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka
    shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake;
    ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi
    wake ulinitia mashaka.
    Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga
    hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni.
    Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba
    maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini….
    Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana
    nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua....
    nikapand ngazi. Mary alifungua mlango nikamwambia,
    ‘Samahani, Mary, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’.
    Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa
    changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake
    kichwani kwangu. ‘Samahani, Mary, nimesema sitaki
    kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na
    furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu,
    mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani.
    Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu
    nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu,
    nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo
    kitakapotutenganisha.’
    Ikawa kama Mary alizinduka usingizini. Akanizaba kibao
    cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia.
    Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye
    duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili
    ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye
    kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila
    asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenganisha”.
    Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu,
    tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani,
    nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.
    Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani
    kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu
    nilihamishia akili yangu kwa Mary. Alijua kwamba
    angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na
    mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.
    Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume
    mwema.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI