• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 7 June 2017

    MBUNGE COSATO CHUMI ATOA MSAADA WA AMBULANCE NYINGINE JIMBONI KWAKE


    MBUNGE wa Mafinga Mjini, Cosato
    Chumi
    akizungumza na wananchi wa Igohole wakati kukadhi gari la kubebea wagonjwa ambalo amepewa na wizara ya
    Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
    MBUNGE wa Mafinga Mjini, Cosato
    Chumi sambamba na mwenyekiti wa halmashauri ya mji wa mafinga Charles Makoga wakikata utepe wa gari la kubebea wangonjwa la kituocha afya cha Igohole
     hawa ni baadhi ya wananchi waliojitokeza wakati wa kupokea msaada wa gari hilo la kubebea wagonjwa lilotelewa na mbunge wa Mafinga Mjini, Cosato
    Chumi kwa kushirikiana na wizara ya
    Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
    Na Fredy Mgunda,Mafinga


    MBUNGE wa Mafinga Mjini, Cosato
    Chumi kwa kushirikiana na wizara ya
    Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wametoa msaada wa gari la
    kubeba wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya matumizi ya kituo cha afya cha Igohole
    ya wilayani Mufindi, mkoani Iringa iliyopo katika jimbo lake hilo.
     
    Gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser lilikabidhiwa kwa
    uongozi wa halmashauri ya mji wa Mafinga inayosimamia uendeshaji wa kituo hicho
    katika mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Igohole, mjini Mafinga.
     
    Akikabidhi msaada huo Chumi alisema;
    “napenda ifahamike kwamba gari hilo limenunuliwa na wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
    Uadilifu na uaminifu kwa serilikali ndio umetufanya tushirikiane vyema katika
    mambo mengi kwa faida ya wananchi wa jimbo langu la Mafinga.”
     
    Alisema gari hilo la wagonjwa
    ni rafiki kwa wagonjwa na wajawazito kwa kuwa lina vifaa tiba vinavyoweza
    kutumika kutolea huduma wakati wakipelekwa hospitalini.
     
    Baada ya kukabidhi gari hilo, Chumi
    ambaye ni mbunge wa kwanza wa jimbo hilo jipya, mkoani Iringa alikumbusha
    vipaumbele vyake kwa wapiga kura wake kuwa ni kuhakikisha jimbo la mafinga
    mjini linapata huduma bora ya maji, elimu, afya na miundombinu ya barabara.
     
    Akishukuru kwa msaada huo, Mganga
    Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Dk Innocent Mhagama alisema kabla ya
    msaada huo, kituo hicho cha afya kilikuwa hakina gari hata moja la kubeba
    wagonjwa.
     
    “Pamoja na kuhudumia hospitali hiyo
    ya wilaya, kurikuwa na magari mawaili tu ambayo yalikuwakihudumia vituo vingine
    18 vya kutolea huduma katika wilaya hiyo hivyo,” alisema Mhagama.
     
    Alisema kupatikana kwa gari hilo
    jipya kutasaidia kuboresha huduma hiyo  kwa kuokoa maisha ya wagonjwa na
    maisha ya mama na mtoto ambayo ni kipaumbele katika utoaji wa huduma za afya.
     
    Akizungumzia huduma ya mama na mtoto
    katika hospitali hiyo ya wilaya, Dk Mhagama alisema kwa wastani wajawazito 500
    wanajifunga kila mwezi hospitalini hapo.
     
    “Kati yao wajawazito zaidi ya 100
    huwa wanapata huduma za dharula huku wastani wa wajawazito 10 wakipatiwa huduma
    za rufaa,” alisema dr Mhagama.
     
    Naye
    mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Mafinga, Charles Makoga alisema halmashauri
    yake kwa kushirikiana na mbunge huyo itahakikisha inatekeleza ahadi mbalimbali
    zilizotolewa na Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Dk John Magufuli, mbunge na
    madiwani ili kuboresha huduma kwa watu wake

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI