Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala
Bora, Angella Kairuki, ameanza ziara yake Mkoa wa Dar es Salaam kwa
lengo kuzifahamu changamoto mbalimbali za watumishi na kutoa maelekezo
ya kutatua kero hizo.
Katika
ziara yake ambayo ameanza na Wilaya ya Temeke Waziri Kairuki ameagiza
uanzishwaji wa vituo vya kusaidia upatikanaji wa huduma kwa wakati
maarufu kama 'One Stop Center' katika idara ya Mamlaka ya Mapato (TRA)
na idara ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), ili
kuongeza ufanisi wa kazi na ukusanyaji wa kodi kwa wakati, halkadhalika
uwepo usajili wa biashara kwa haraka ambapo itasaidia katika Mpango wa
Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania maarufu kama “MKURABITA”
"Hizi
One Stop Center ni muhimu sana baadhi ya Mikoa imeanza kunufaika na
uanzishwaji wake ikiwemo Mkoa wa Morogoro ambapo imepelekea ukusanywaji
wa mapato kwa haraka na kuchochea shughuli za maendeleo" alisema Waziri
Kairuki.
Katika
hatua nyingine Waziri Kairuki ametoa msisitizo kwa Maafisa Utumishi
kuhakikisha serikali inapotoa vibali vya kazi, hawaajiri watu bila
kujiridhisha na taarifa zao za kielimu ili kuepuka suala la watumishi
wenye vyeti feki, ambapo ameeleza kuwa kwa mujibu wa taarifa
iliyowakilishwa na Katibu Tawala Msaidizi Michael Mungaya wa Mkoa wa Dar
es Salaam imeeleza kuwa watumishi 937 wanavyeti feki na katika hao 421
wameleta vyeti pungufu, ni vyema umakini ukafanyika ili kuondoa hasara
kwa taifa.
Waziri
Kairuki ameongeza kuwa mfumo wa taarifa za watumishi (Lawson)
utasaidia katika kuhakiki taarifa zao ikiwemo kujua mahala walipo
watumishi na wanafanya nini, hivyo kupitia mfumo huo watajiridhisha na
kufanya maamuzi sahihi kwa watumishi.
Pia
Waziri Kairuki amewasihi watumishi kutoa huduma bora kwa wananchi bila
ya ubaguzi wa aina yeyote na kutenda haki kwa kufanya kazi kwa weledi na
kuacha kufanya kazi kwa mazoea, halikadhalika kuepuka suala la kutoa au
kupokea rushwa.
Kwa
upande wake Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva amemuomba Waziri
Kairuki kuhakikisha kuwa watumishi wanapewa makazi jirani na vituo vyao
vya kazi ili kuboresha ufanisi kazi na uwepo wa usalama na ulinzi, pia
DC Lyaniva amemueleza Waziri Kairuki kuwa wameweza kuongeza saa limoja
la ziada la kuwahudumia wananchi katika wiki ya utumishi wa umma
iliyofanyika tarehe 16 mpaka 23 mwezi June.
No comments:
Post a Comment