• Breaking News

    ..

    ..

    Sunday 30 July 2017

    MAMA NAMAINGO ‘AWAFUNDA’ AKINAMAMA WA GREEN VOICES KILIMOBIASHARA NA UJASIRIAMALI

    Mkurugenzi wa Namaingo, Biubwa Ibrahim
    Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba, akiwapa majukumu washiriki wa warsha hiyo.
     
    MKURUGENZI
    Mtendaji wa kampuni ya Namaingo Business Agency, Biubwa Ibrahim, amewataka
    akinamama wanatekeleza mradi wa Green Voices Tanzania kuwa wabunifu na kutokata
    tamaa katika shughuli wanazozifanya.
    Akizungumza
    wakati wa kufunga semina ya siku sita ya mafunzo yaliyowashirikisha akinamama
    15, Biubwa alisema kwamba, ubunifu, jitihada na kutokata tamaa ndiyo silaha
    kubwa katika mafanikio, huku akiwahimiza watafute fedha bila kuchoka.
    “Lazima
    muwe wabunifu, halafu ni dhambi kubwa kukata tamaa bali mnatakiwa kuongeza
    jitihada katika mradi yenu,” aliwahimiza.
    Aidha,
    alisema kwamba, mafanikio yoyote hayawezi kuja kwa siku moja, hivyo wanapaswa
    kuwa wavumilivu daima ili waweze kufanikiwa.
    Akinamama
    hao wa Green Voices wanatekeleza miradi mbalimbali ya kilimo inayoendana na
    mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi, ambayo
    inadhaminiwa na taasisi ya Women for Africa Foundation ya Hispania inayoongozwa
    na makamu wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Bi. Maria Tereza Fernandes de la Vega.
    Biubwa
    alisema, wajasiriamali wengi wanaposhindwa kuona faida ya shughuli
    wanazozifanya huvunjika moyo mapema, lakini hilo lisiwe kikwazo kwao kwani
    wanapaswa kukaa chini na kutafakari njia mpya ya kuendesha biashara ama miradi
    yao.
    “Inabidi
    kujiuliza wewe mwenyewe kama hapo ulipo ndipo mahali sahihi, vinginevyo usife
    moyo unapoona mambo hayaendi, bali angalia wapi ulipokosea na ujipange upya
    halafu utaona matokeo yake,” alisema.
    Akaongeza:
    “Mimi nilianza na mtaji wa shilingi elfu nne tu, nimepitia changamoto nyingi
    ikiwemo kudhulumiwa fedha, lakini katu sikukata tamaa nimeendelea kupambana na
    mpaka sasa kupitia kampuni yangu nimeweza kusajili wakulima 400,000 nchi
    nzima.”
    Mwanahabari mshiriki wa mradi wa Green Voices, Farida Hamisi, akipokea cheti kutoka kwa Alicia Cedaba, Mratibu wa Green Voices kutoka Hispania. Katikati ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Olomi kutoka taasisi ya IMED.
     
    Mradi wa
    Green Voices unatekelezwa nchini Tanzania pekee, ambapo akinamama 10 kati ya 15
    wanaendesha miradi mbalimbali ya kilimo, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mboga
    na matunda pamoja na utengenezaji wa majiko rafiki katika jitihada za kupambana
    na mabadiliko ya tabianchi.
    Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa
    watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – Majiko
    Banifu
    ), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – Usindikaji
    wa Muhogo na Mtama
    ), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – Kilimo
    cha Uyoga
    ), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – Ufugaji
    wa Nyuki
    ), na Esther Muffui (Morogoro – Ukaushaji
    wa Mboga na Matunda
    ).
    Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – Majiko
    ya Umeme-Jua
    ), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – Kilimo
    na Usindikaji wa Viazi Lishe
    ), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – Ufugaji
    wa Nyuki
    ), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – Kilimo
    Hai cha Nyanya na Mbogamboga
    ), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo
    cha Matunda).
    Mradi huu wa Green Voices ambao mwaka huu uko
    katika awamu ya pili, ulizinduliwa Julai mwaka 2016 na Makamu wa Rais wa
    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.
    Katika awamu ya pili kinamama hawa
    wameendelea kuboresha kilimo cha mazao yao kinachozingatia uhifadhi wa
    mazingira na mabadiliko ya tabia nchi katika mikoa sita nchini.
    “Pamoja na kilimo, Mradi wa Green Voices
    umaeandaa mafunz mbalimbali ya kuongeza ujuzi katika kilimo (climate smart
    agricultura) pamoja na mafunzo ya jinsi ya kuandaa mazao au bidhaa
    wanazozalisha kupitia kilimo,” alisema Mratibu wa Green Voices nchini Tanzania
    Secelela Balisidya.
    Katika kutekekelza hilo, Green Voices kupitia
    mfadhili wake, Women for Africa Foundation, walishiriki katika mafunzo
    mbalimbali ya Mbinu bora za kuweka nembo na kufungasha bidhaa za vyakula,
    Viwango vya Ubora, na Kanuni za uchakataji wa vyakula.
    Mafunzo hayo ambayo yalifanyika Julai 16 -22,
    2017 yalizinduliwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani
    Jaffo, ambaye aliahidi kuwapa ushirikiano akina mama hao.
    Utengenezaji bidhaa na ufungashaji
    Kwa siku
    sita baada ya kuzinduliwa kwa mafunzo, akinamama hao walijifunza kuhusu Mchango
    wa kilimo katika mabadiliko ya tabianchi, Jinsi ya kuweka mazingira bora ya
    umwagiliaji, Mikakati ya biashara katika ujasiriamali wa kilimo, Utafutaji wa
    rasilimali na mkakati wa kuongeza mtaji, Ukuzaji wa mtaji kupitia Vicoba, na Mbinu
    za uongozi.
    Akinamama
    hao walipata fursa ya kutembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la
    Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo ilikutana na wajasiriamali walio
    katika hatua za juu za kufungasha na kuuza bidhaa zao, ambapo walipata nafasi ya
    kubadilishana nao mawazo ili kuongeza ujuzi wao.
    Katika
    mafunzo hayo, Linus Gedi ambaye ni mtaalam wa ubora wa chakula na viwango kabla
    ya kuvipeleka sokoni, aliwaeleza washiriki kwamba ni muhimu kufungasha na
    kuweka nembo kwani inasaidia kuhifadhi bidhaa na inarahisisha  mteja kutambua hiyo ni bidhaa ya aina gani,
    imetengenezwa wapi na ina mchanganyiko gani.
    Akinamama wanaotekeleza mradi wa Green Voices walipotembelea Ofisi za SIDO jijini Dar es Salaam.
     
    “Ni
    muhimu sana kuhakikisha chakula hakisababishi maradhi, lakini pia kinafikia
    malengo ya walaji, hii huepusha sumu kwenye chakula, mchanganyiko usiofaa,
    upotevu wa chakula, kupoteza bidhaa na kuepukana na masuala ya kisheria,”
    alisema Linus.
    Alisema
    uzalishaji wa chakula unatakiwa kuzingatia mbinu bora za uzalishaji na pamoja
    na usafi.
    Aidha,
    aliwataka kuzingatia ubora, usafi na viwango vya chakula wanachozalisha ili
    kifikia malengo ya walaji.
    Kwa upande
    wake, Richard Jackson akielezea umhimu wa kunadi bidhaa, alisema ni lazima kuwa
    na mikakati imara ya masoko ili kuhakikisha mjasiriamali anapata faida.
    Alisema ni
    vizuri kujua wateja maalum na wateja wa ujumla na nini hasa wanahitaji ikiwa ni
    pamoja na namna ya kuwafikia.
    “Ni lazima
    kujua kati ya wanaohitaji bidhaa zako, ni nani ambao siyo wateja wako walengwa
    na kwa nini wateja wanunue bidhaa zako na siyo kwa washindani wako?
    Lazima ujue tabia zao na ukubwa wa soko lako,” alisema Jackson.
    Aidha, alisema ni muhimu kuwajua wateja wako ili kuelewa
    mahitaji yao na kwa nini wananunua bidhaa wanazonunua pamoja na kutambua mambo
    yanayowaudhi ili usiwakwaze.
    Kwa upande wa uchangishaji fedha na kutafuta
    mitaji kwa biashara na kilimo, Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota
    Likokola, alieleza jinsi mfumo wa VICOBA Endelevu unavyoweza kuwasaidia
    kinamama wa Green Voices kupata mitaji ya kuendeleza miradi yao.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI