• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 13 July 2017

    Mbunge wa Mkuranga kufunga Tamasha la SHIWATA.

    indexTAMASHA la Sanaa na Michezo la Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)linaanza kesho Ijumaa jijini Dar es Salaam ambako wasanii zaidi ya 600 wanatarajia kushiriki.
    Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa SHIWATA,Cassim Taalib na kuongeza kuwa mgeni rasmi atakayegungua semina hiyo ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Godfrey Mngereza.
    Taalib alisema Mngereza atashuhudia michezo mbalimbali itakayoneshwa na wasanii na
      wanamichezo na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega atafunga tamasha hilo Jumamosi.
      Alisema tamasha hilo ambalo awali lilikuwa lifanyike kijiji cha Wasanii
    Mkuranga limehamishiwa jijini Dar es Salaam sababu kubwa ya kuhamisha
      tamasha hilo ni kutokana na mvua ya msimu uliopita kuharibu barabara ya
    kwenda kijijini.
      Taalib alisema tamasha hilo sasa  litafanyika kwa siku mbili kuanzia kesho Ijumaa Julai 14.7.2017 na kuhitimishwa Jumamosi Julai 15 mwaka huu katika
      viwanja vya Chuo cha Uhazili, splendid Ilala Bungoni.
      Alisema mpaka sasa wameanza kupokea wanamichezo kutoka sehemu
    mbalimbali kama vile Mkuranga, Kibiti, Zanzibar na Morogoro ambao washiriki tamasha hilo.
      Baadhi ya michezo ambayo itafanyika ni sarakasi, Tae kwon-do, muziki
      wa dansi, ngumi, soka,rede,muziki wa asili,wu shuu,ngoma,singeli na michezo
      mingine.
      Alisema kampuni ya SBC wanaotengeneza soda za Pepsi ndiyo
    wadhamini wakuu wa tamasha hilo na kuongeza kuwa milango iko wazi kwa
      wadhamini wengine kujitokeza.
    Akizungumzia ujenzi wa nyumba zao kijijini alisema mgawo na
      makabidhiano ya nyumba 14 ndogo,kubwa tatu na viwanja 35 vilivyopimwa
      utafanyika Julai 16 siku moja baada ya kumalizika tamasha hilo.
      Alisema kuanzia sasa wanachama wanaotaka kujenga nyumba zao wenyewe
      wawasiliane na Shiwata ili wapewe maelekezo na utaratibu wa kufanya usafi
    kwenye makazi yao.
    Mwenyekiti alisema utaratibu wa kulipia umeme kupitia mpango wa umeme
      vijiijini (REA)unaendelea na mikakati ya kukarabati barabara ya kufika
      kijijini unafanyika.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI