Aliejifanya dokta feki akamatwa tena Amana akijifanya daktari na wakala wa ajira
Daktari feki aliyewahi kukamatwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jully 19 mwaka huu amekamatwa tena leo akijifanya daktari katika hospitali ya Amana jijini Dar es salaam.

Akizungumza Mara baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Msimamizi wa huduma kwa watu wenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi Dkt SHANI MWALUKA amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna mtu anajifanya daktari ambaye aliwaahidi wagonjwa kuwa angewapatia huduma na akataka apewe fedha ndipo uongozi wa hospitali hiyo ulipomwekea mtego na kumnasa daktari feki huyo ambaye hakuwa na kielelezo chochote kuwa yeye ni mtumishi wa hospitali ya amana.
Nao baadhi ya watu ambao wamewahi kutapeliwa na daktari huyo wamesema kuwa amekuwa akijitambulisha kama Dk Abdalah Omary na aliwaahidi kuwasaidia kupata kazi katika mahoteli na makampuni ya ujenzi hiyo na kupewa kiasi cha shilingi laki nane ambazo aliwatapeli na baadaye kuwataka wakutane Amana hospitali Leo ndipo walipomwekea mtego huo na kufanikiasha kunaswa kwake

Akizungumza Mara baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo Msimamizi wa huduma kwa watu wenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi Dkt SHANI MWALUKA amesema walipata taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuwa kuna mtu anajifanya daktari ambaye aliwaahidi wagonjwa kuwa angewapatia huduma na akataka apewe fedha ndipo uongozi wa hospitali hiyo ulipomwekea mtego na kumnasa daktari feki huyo ambaye hakuwa na kielelezo chochote kuwa yeye ni mtumishi wa hospitali ya amana.
Nao baadhi ya watu ambao wamewahi kutapeliwa na daktari huyo wamesema kuwa amekuwa akijitambulisha kama Dk Abdalah Omary na aliwaahidi kuwasaidia kupata kazi katika mahoteli na makampuni ya ujenzi hiyo na kupewa kiasi cha shilingi laki nane ambazo aliwatapeli na baadaye kuwataka wakutane Amana hospitali Leo ndipo walipomwekea mtego huo na kufanikiasha kunaswa kwake

No comments:
Post a Comment