• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 9 August 2017

    RC MAKONDA AKAMILISHA JUKUMU LA BUNJU B


    Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam mhe. Paul Makonda ametoa siku tatu kwa mhandisiwa wa umeme wa Manispaa ya Kinondoni kuwasilisha mchoro wa miundombinu ya umeme ya soko la Bunju B ili  Tanesco iweze kuunganisha umeme katika soko hilo.

    Mhe. Makonda  ametoa agizo hilo alipo kuwa akisikiliza kero za wananchi katika viwanja vya soko hilo baada ya kuelezwa na mhandisi wa Tanesco mkoa wa  Tanesco  Kinondoni kuwa manispaa waliagizwa kupeleka  mchoro tangu mwezi April mwaka huu lakini hadi leo hawajafanya hivyo, jambo ambalo limesababisha usumbufu mkubwa kwa wafanya biashara wanaofanya biashara sokoni hapo.

    Pamoja na hayo Rc Makonda amewataka watumishi na watendaji serikali mkoani humo kufanya kazi kwa bidii na kushughulikia kero na changamoto za wananchi ilikuweza kuleta maendeleo na kutekeleza ilani ya CCM.

    “watendaji tuna mchosha Rais kwa mambo madogomadogo ambayo tungeweza kuyamaliza sisi huku chini yeye tuka mwacha akashughulikia mabo makubwa ,huyo huyo ashughulikie makinika , Mafisadi , Bomba la Mafuta halafu sisi tuwe tumekaatu haiwezekani lazima tuwajibike “alisema Makonda

    Kwa upande wao wanachi hao wakizungumza ma mhe. Makonda katika mkutano wa hadhara wamesema kuwa tatizo kubwa linalo kabili sokohilo ni ukosefu wa umeme,Maji ya kutosha, uchache wa matundu ya choo  na kero ya baadhi ya wafanya biashara kukimbilia kwenda kufanya kazi barabarani.

    Wanachi hao wameomba soko hilo kufanywa sehemu muhimu ya ya kuuza mazao na bidha kwa jumla ili kupunguza msongamano katika masoko mengine,na kulifanya soko hilo kuwa enemuhimu la kibiashara pia itasaidia kuwatoa wote wanaofanya biashara katika maeneo ya pembezoni mwa barabara.

    Aidha wananchi hao wameeleza kero ya kupasuka kwa mabomba ya maji (DAWASCO) ambapo Mhandisi wa Dawasco Bw. Aron Joseph ambapo amesema kuwa hali hiyo ya kupasuka ni inatokana na masuala ya kiufundi ambapo kumekuwa na presha (Msukumo) kubwa wa maji kutokana na ukosefu wa matanki ya kutosha.

    Hata hivyo Mhandisi Aron ametoa siku mbili kwa Meneja Mkoa bagamoyo Meneja wa DAWASCO kanda ya Tegeta na Bagamoyo Edga Zawa pamoja na Meneja Mkoa Tegeta Ambokile kuhakikisha mabomba yote yanayomwaga maji yanazibwa haraka ili kuondoa keo kwa wananchi hao.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI