• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday 30 September 2017

    10 wafariki baada ya ndege ya kijeshi kuanguka DR Congo



    Picha ya ndege ya kijeshi ilioanguka
    Picha ya ndege ya kijeshi ilioanguka
    Ndege ya kijeshi imeanguka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kuwaua abiria wote.
    Maafisa wa maswala ya angani wamesema kuwa zaidi ya watu 10 wamefariki baada ya ndege hiyo kufeli kupaa vizuri kutoka uwanja wa ndege wa N'djili katika mji mkuu wa Kinshasa na kuanguka katika makaazi ya Nsele.
    Haijabainika iwapo kuna watu wowote waliouawa ama kujeruhiwa ardhini.
    Mkurugenzi wa uwanja wa ndege wa Kinshasa amesema kuwa ndehe hiyo ilikuwa ikibeba mizigo na kwamba haikuwa na abiria wowote.
    Ripoti nyengine zinasema kuwa baadhi ya wanajeshi waliuawa
    Chanzo bbc swahili.com

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI