• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 12 September 2017

    LHRC wazungumza hili kuhusu Rais Magufuli

    Na Ahmed Kombo     
    Watetezi wa haki za binadamu kwa umoja wao wametaka watu wasiojulikana waweze kuchukuliwa hatua za kiusalama mara moja 
    ili kubaini wahalifu hao wanajihusisha na vitendo vya kikatili dhidi
     ya watu mbalimbali na kuzuia hali hiyo isiendelee kutokea tena.

    Akisoma tamko hilo leo kwa niaba ya wadau  wengine  jijini Dar es Salaam mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu DAKTA  HELEN KIJO-BISIMBA amesema katika kipindi  kifupi kumekuwa na matukio kadhaa ya ukiukwaji wa misingi ya haki za binadamu yakiambatana na vitendo vya mauaji,utekwaji na manyanyaso kwa watetezi wa haki za binadamu,viongozi wa kisiasa,maafisa wa polisi na wananchi matukio ambayo yameendelea kuleta hofu baina ya wananchi kuhusu hali ya usalama nchini.

    Dakta KIJO-BISIMBA amesema wadau pamoja na jumuiya ya watetezi wa haki za binadamu wanasikitishwa na vitendo hivyo huku wakiwaomba viongozi wa dini wachukue hatua madhubuti kukemea matukio kama hayo kwa nguvu kwani mwisho wa matukio kama haya ni kuvunjika kwa amani nchini.


    Katika hatua Lhrc  kimefurahishwa na kauli ya Rais Dakta  MAGUFULI ya kuonyesha kutofurahia adhabu ya kifo,kauli ambayo inalandana na juhudi za haki za binadamu za kupinga adhabu ya kifo kwa vile inadhihirisha kuwa adhabu hiyo haina faida na haitekelezeki nchini.
    Kwa mujibu wa ripoti ya haki za binadamu Tanzania 2016, mpaka kufikia mwaka 2015 jumla ya watu 472 wamehukumiwa kunyongwa wakati mara ya mwisho kutekelezwa kwa adhabu hiyo ilikuwa mwaka 1994.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI