• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 12 September 2017

    RC Makonda kuiangukia TRA. amegundua ujanja unaofanyika ,soma zaidi hapo.

    Baadhi ya wafanyabiashara wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, mhe paul Makonda hayupo  pichani katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es salaam leo.( picha na Camera ya Mwambawahabari)
    Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam mhe Paul Makonda ,meitupia lawama Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA mkoa wa kodi Ilala  kwa tabia ya kuwavizia wafanyabiashara wakati wa ukusanyaji mizigo, na baadhi yao hudai pesa kinyume cha sheria (rushwa)  ili kusamehewa faini wanayotozwa na Mamlaka hiyo.


    Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda katika mkutano wake na Wafanyabiashara wa Dar es aliouitisha kuzungumza nao  ili kutatua kero zao.

    "Ninaushahidi wa clip hapa m fanya kazi wa TRA akiomba milioni 100 katika duka la mfanyabishara biashara, na ninyi wafanyabiashara Nawaomba  mfunge camera katika maduka yenu ili tuwabaini hao wanao ombarushwa". Amesema Makonda.

    Katika hatua nyingine Makonda  amewaomba wafanyabiashara kuchangia kampeni yake ya  ujenzi wa vyoo vya shule na Ofisi za walimu  katika mkoa wa Dar es Salaam, ambapo pia aliwataka na kuunda Kamati  kwaajili ya kujadili maendeleo yao kibiashara na changamoto za kazi yao.

    Mkuu wa kodi  mkoa wa kodi Ilala Abdull Mapembe, amesema Kuna baadhi ya wafanyabiashara wa sio waaminifu huzunguka na lisiti moja, pia huandika bei tofauti na thamani hali si ya bidhaa katika risiti ya kielektroniki.
                                                     
    "Ikiwa Mfanyabiashara atabainika kuwepo kulipa kodi au kuandika lisiti kwa kuficha gharama hali si ya mazoez ya bidhaa atachukuliwa hatua za kisheria." Amesema Afisa huyo.

    Katika upande mwinginw kumezuka lawama kwa wafanyabiashara wa vifaa na spea za magari kwa kusema jeshi la polisi limekuwa likichukua spea hizo kwa kusema miongoni mwa vifaa hivyo ni vya wizi hali ambayo wafanya biashara hao wamesema hakuna ukweli wowote ambapo wamemwomba mhe. Makonda kutoa utaratibu kwa Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam  ilikurudisha vifaa hivyo vya magari ambavyo havijachukuliwa na wananchi , nakusema kuwa hii inaonyesha kuwa  havikuwa vya wizi hivyo ni haki kurudishiwa wenyewe.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI