Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Mhe. Seif Sharif Hamad leo
Septemba 26, 2017 ameingia jijini Nairobi Kenya kwenda kumjulia hali
Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama Cha Wanasheria Tanganyika
(TLS), Tundu Lissu ambaye alipigwa risasi.
Mwenyekiti wa kamati ya muda ya uongozi CUF, Julius Mtatiro
amethibitisha hilo na kusema kuwa kiongozi huyo na baadhi ya viongozi wa
CUF wamewasili nchini Kenya kwa ajili ya kwenda kumuona Tundu Lissu.
"Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Mhe. Seif Sharif Hamad ameingia
jijini Nairobi kumjulia hali Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa
Chama cha Wanasheria Tanganyika Mhe. Tundu Antipas Lisu (leo) ambaye
amelazwa Hospitali ya Nairobi" alisema Julius Mtatiro
No comments:
Post a Comment