Rais Donald Trump amesaini sheria mpya ya kuongeza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini juu ya mpango wake wa nuklia.
Waziri wa fedha wa Marekani ameidhinisha vikwazo hivyo dhidi ya
makampuni ya fedha yanayofanya biashara zake ndani ya Korea Kaskazini.Rais Trump pia amesema kuwa Benki Kuu ya Uchina iliagiza benki nyingine za Uchina kuacha kufanya biashara na Korea Kaskazini.
Marekani yatishia kuiadhibu Korea Kaskazini
Malaysia yaishutumu Korea Kaskazini
Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa
Hatua hii inakuja katika kipindi cha chini ya wiki mbili baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo ipya dhidi ya taifa hilo kwasdababu ya jaribilo lake la hivi karibuni la nuklia.
Hali ya wasi wasi imetanda katika kipindi cha wiki za hivi karibuni kutokana na hatua ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu, licha ya shinikizo kutoka kwa mataifa tajiri zaidi duniani.

No comments:
Post a Comment