Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi.
………………………………………………………..
Wananchi wa Vijiji vya Titu,
Kisangire, Kihare, Kolesa na vikumburu wanatarajia kupata ukombozi
kupitia mpango kabambe wa ujenzi wa barabara ya Chole – Titu – Kihare
hadi vikumburu utakaoanza muda wowote ndani ya mwaka huu.
Barabara hiyo imekuwa na
changamoto kubwa miaka yote kutokana na kukosekana kwa daraja katika mto
unaotenganisha kijiji cha Titu na Kisangire pamoja na kuwepo kwa
tifutifu kubwa kwa eneo lote la barabara kitendo kinachosababisha
wananchi wa maeneo hayo kupata shida kubwa ya kusafiri.
Katika ajenda ya kusukuma
maendeleo, Mbunge wa Jimbo hilo Selemani Jafo amehangaikia kuboresha
barabara hiyo na kufanikiwa kupata ufumbuzi kwa wakazi wa maeneo hayo
kwani barabara hiyo katika kupindi kifupi kijacho itajengewa daraja
kubwa katika mto uliopo katika kijiji cha titu na kuirekebisha barabara
yote kwa kuiwekea kifusi, makalavati na mifereji ili kuruhusu magari
kupita kipindi chote cha mwaka.
Ujenzi huo unatarajia kugharimu
zaidi ya shilingi bilioni 1.5 ambapo kazi hiyo inatarajiwa kutangazwa
wakati wowote kuanzia sasa.
Katika kufanikisha hilo, Jafo amewataka wananchi wote kushikamana ili kuharakisha maendeleo wilayani kisarawe
No comments:
Post a Comment