• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 25 October 2017

    DAS CHINTIKA: WALIMU TUMIENI KONDOMU ILI KUPUNGUZA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

     Katibu tawala wa wilaya ya Iringa Joseph Chintinka akiwa kwenye mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Iringa manispaa akizungumza na baadhi ya walimu walihudhuria mkutano huo. 
    Baadhi ya walimu waliokuwa wanaimba wimbo wa walimu wakati wa mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Iringa manispaa uliofanyika katika ukumbi wa chuo kikuu huria tawi la Iringa.
     
    Na Fredy Mgunda,iringa. 
     
    Walimu wa halmashauri ya
    manispaa ya Iringa wametakiwa kutumia kondomu ili kujikinga na magonjwa ya
    zinaa amboya yamekuwa yakipunguza nguvu kazi ya taifa.
     
    Hayo yamesemwa na katibu
    tawala wa wilaya ya Iringa Joseph Chintinka wakati wa mkutano mkuu wa chama cha
    walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Iringa manispaa.
     
    Chintinka alisema kuwa
    kumekuwa na ongezeko la waathirika wa ugonjwa wa ukimwai kutokana na kufanya
    mapenzi bila kutumia kondomu.
     
    “Jamani hapa Iringa kuna
    tatizo kubwa la ugonjwa wa ukimwi hivyo niwaombe walimu wangu tutumie kondomu
    ili kujiepusha na gonjwa hili vinginevyo vizazi vyetu vyote vitaambukizwa
    ukimwi” alisema Chintinka
     
    Chintinka alisema njia ya
    kuwa salaama kuepukana na gonjwa hili ni kujikinga kwa kutumia kondomu maana
    hata watoto wetu wameathirika kutokana na wazazi kutokuwa makini na matumizi ya
    kinga
     
    “Naombeni tuwakinge hawa watoto
    wetu ambao wameathirika ili wasiwaambukize watoto wengine maana bila hivyo
    tutakuwa na kizazi kilichoathirika” alisema Chintinka
     
    Aidha Chintinka aliwaomba
    walimu walioathirika kujitokeza ili kupewa lishe ambayo inatolewa na serikali
    bure hivyo walimu wametakiwa kujitokeza na kuweka wazi kwa mwagili wake ili
    aweze kupata mgao wa pesa za lishe.
     
    “Jamani walimu fungu la
    lishe kwa walimu walioathirikia ni nono kweli naombeni walimu mjitokeze ili
    mfaidi fungu hili nono maana mimi nafahamu sisi ndio tunaotenga naombeni
    fikisheni ujumbe huu kwa walimu wengine ambao hawajafika hapa” alisema Chintinka
     
    Chintinka aliwataka
    watumishi wanaotoa siri za watumishi walioathirika kuacha tabia hiyo mara moja
    ili kuwaweka huru waathirika na wengine waweze kujitokeza na wapate lishe
    iliyotengwa na wilaya.
     
    Kwa upande wake mwenyekiti
    wa chama hicho manispaa ya Iringa MWL. Zawadi Mgongolwa alikiri kuwepo kwa
    viongozi wa sekta hiyo ambao wemekuwa wakitoa siri za walimu na watumishi
    walioathirika na ugonjwa wa ukimwi.
     
    Kwa kweli mgeni rasmi
    umeongea ukweli kero kubwa kwa walimu ni kutolea siri nje kitu kinachowafanya
    walimu waathirika kujificha na maradhi yao” alisema Mgongolwa
     
    Naye katibu wa chama cha
    walimu wilaya ya Iringa mwl. Fortunata Njalale alimpongeza mgeni rasmi kwa
    ujumbe wake ambao umekuwa faraja kwa walimu na kuwaongezea hali ya kwenda
    kufanya kazi ya uwalimu kwa kujituma na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wao.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI