Hata hivyo Dakta Kolimba amesema katika maadhimisho hayo kutakuwa na gwaride maalum pamoja na kupandishwa bendera ya umoja wa mataifa , wageni mbalimbali watakuwepo wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali ,vyombo vya usalama, wanafunzi pamoja na wananchi.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo itakuwa ''MAENDELEO YA VIWANDA YAZINGATIWE,UTUNZAJI WA MAZINGIRA NA MAENDELEO ENDELEO''
Kwa upande wa mwakilishi wa umoja wa mataifa Alvaro Rodrigez amesema wanaipongeza serikali ya Tanzania kuendelea kuleta maendeleo ya nchi ,uhifadhi wakimbizi wengi na wataendelea kushirikiana na serikali na wadau wa maendeleo nchini kwa ajili ya watanzania.
Mwandishi Apolonia Kisite
No comments:
Post a Comment