![]() |
| Aliondika baada ya wachezaji wa timu ya San Francisco 49ers haikusimama wakati wa wimbo wa taifa |
Makamu wa rais wa
Marekani Mike Pence, ameondoka kutoka kwa mechi ya kandanda ya NFL
nchini Marekani, baada wachezaji kukataa kusimama wakati wa kuchezwa kwa
wimbo wa taifa wa Marekani.
Bw. Pence alisema kuwa hatakuwa
kwenye warsha ambayo haiheshimu wanajeshi wa Marekani au bendera baada
ya kuondoka kwenye mechi iliyokuwa ikichezwa katika jimbo nyumbani kwake
huko Indiana.Rais Donald Trump aliandika katika mtandao wa twitter kuwa alimuomba Pence kuondoka ikiwa wachezaji wangepiga magoti.
Kupiga magoti wakati wa mechi za NFL imekuwa njia ya kupinga ubaguzi wa rangi
Mike Pence aliondika baada ya wachezaji wa timu ya San Francisco 49ers haikusimama wakati wa wimbo wa taifa
Trump amewakosoa wachezaji vikali na kuitaka NFL kuwapiga marufuku.
"Niliondoka katika mechi ya leo kwa sababu rais Trump na mimi hatutakubali warsha yoyote ambayo haieshimu wanajeshi wetu, bendera yetu au wimbo wetu wa taifa," Pence aliandika kwenye twitter siku ya Jumapili.
Aliondoka baada ya wachezaji wa timu ya San Francisco 49ers haikusimama wakati wa wimbo wa taifa kabla ya mechi dhidi ya Indianapolis Colts.
Awali Bw. Trump alisema kuwa matamshi yake ya kukosoa hatua za NFL hayakuhusu kwa vyoyote vile suala la rangi

No comments:
Post a Comment