• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday 31 October 2017

    Nane wafa katika shambulizi la gari Marekani

    Marekani
    Image captionShambulizi nchini Marekani baisikeli na miili ya watu ilitapakaa ardhini
    Meya wa mji wa New York, Bill De Blasio, amearifu kwamba watu nane wamefariki dunia na zaidi ya watu kumi na wawili wamejeruhiwa na gari iliyopamia waendesha basikeli mjini humo.
    Bill amelielezea tukio hilo ni ugaidi wa namna yake kwa umati wa watu kupaamiwa na kuzua hofu mjini humo.
    Kamishna wa polisi wa jiji la New York, James O'Neill, amemuelezea mtu aliyehusika kutekeleza tukio hilo kuwa ni kijana wa miaka ishirini na tisa aliyekuwa anaendesha gari aina ya gari ndogo ya kubebea mizigo aliyokuwa ameikodi.
    Alisema gari hilo liliwagonga waenda kwa miguu na wapanda baiskeli kabla ya kugongana na basi la shule.
    Kwa upande wake bwana O'Neill, amesema kuwa dereva wa gari hilo alitoka kwenye lake na kuanza kuandaa silaha mbili kwa ajili ya shambulizi na kabla ya utekelezaji polisi walimuwahi na kumpiga risasi zilizomjeruhii.
    Marekani
    Image captionGari lililosababisha tukio hilo
    Polisi mjini humo wametoa tamko kwamba wanalichukulia tukio hilo kama shambulizi la kigaidi , Mtuhumiwa wa tukio hilo alichukuliwa na polisi kwa mahojiano zaidi ambao walithibitisha taarifa hizo katika kituo cha Manhattan ya chini.
    Vyombo vya habari nchini Marekani wamenukuu taarifa za polisi kuwa kijana huyo aliamua kuendesha gari hilo katika njia ya waendesha baisikeli iliyoko karibu na Mto Hudson eneo la Manhattan ya chini ,kabla ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi ili kuzuia shambulio alilolipanga

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI