• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 4 October 2017

    SHIRIKA LA WOTESWA LAWANOA WAANDISHI WA HABARI JIJINI MWANZA

    Na George Binagi-GB Pazzo
    Mratibu wa Shirika
    la kutetea haki za watoto wafanyakazi wa majumbani WOTESAWA, Cecilia Nyangasi (pichani juu) amesema shirika hilo limejiwekea mikakati ya kuhakikisha kwamba hadi kufikia
    mwaka 2020 kusiwepo na mtoto chini ya umri wa miaka 18 ambaye ameajiriwa
    kufanya kazi za nyumbani.
     
    Nyangasi
    ameyasema hayo hii leo kwenye mafunzo kwa waandishi wa habari Jijini Mwanza, yaliyolenga
    kuwajengea uwezo wa kusaidia kufikisha elimu katika jamii ili kuondokana na
    mazoea ya kuwaajiri watoto kufanya kazi za nyumbani na hivyo kuwakosefa fursa mbalimbali
    ikiwemo kupata elimu.
     
    Amesema hatua
    hiyo itasaidia kuwanusuru watoto wafanyakazi wa majumbani na ukatili ikiwemo wa
    kingono pamoja na kiuchumi ambapo baadhi yao wamekuwa wakifanya kazi bila
    malipo ama kwa malipo kidogo.
     
    Aidha ametoa
    rai kwa serikali kuboresha sera, mikakati na sheria zinazomlinda mtoto ili
    kuondoa mkanganyiko uliopo ambao unashindwa kutambua bayana umri wa mtoto anayepaswa
    kuajiriwa kwani baadhi hutaja umri wa miaka 14 huku nyingine ikitaja umri wa
    miaka 18.
     
    Nyangasi
    amebainisha kwamba mwaka jana shirika la WoteSawa lilifanya utafiti katika Kata
    nne za Jiji la Mwanza ambazo ni Igogo, Mkuyuni, Butimba na Capriont na kubaini
    kwamba bado watoto wafanyakazi wa majumbani wanakabiliwa na utumikishwaji na
    ili kupambana na hali hiyo shirika hilo lilianzisha mkakati wa kuwafikia watoto
    waajiriwa, waajiri wao pamoja na viongozi wa serikali za mitaa na kuwaelimisha.
     
    Nao
    waandishi wa habari, Moses Mathew kutoka gazeti la Daily News pamoja na Rhoby
    Magira kutoka Redio Afya wamebainisha kwamba mafunzo hayo yatawasaidia kuandika
    habari na makala zinazoielimisha jamii ili kuondokana na mazoea ya kuwatumikisha
    watoto kupitia ajira za majumbani.
     
    Itakumbuka
    kwamba mtoto mfanyakazi wa nyumbani analindwa na sheria kadhaa ikiwemo sheria
    ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009, sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka
    2004 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2017, waraka wa mishahara wa mwaka
    2013 pamoja na katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.
     
     
    Kwa upande
    wa waraka wa mishahara wa mwaka 2013, mfanyakazi wa kazi za nyumbani anapaswa
    kulipwa kiwango cha chini cha mshahara ambacho ni shingili 150,000 iwapo
    mwajiri ni balozi ama mfanyabiashara mkubwa, elfu 80,000 ikiwa mwajiriwa haishi
    kwenye nyumba ya mwajiri wake, elfu 40,000 ikiwa mwajiriwa anaishi kwenye
    nyumba ya mwajiri wake na shilingi 130,000 ikiwa mwajiri ni rai wakigeni ingwa
    waraka huo hautaji mwajiriwa huyo anapaswa asiwe mtoto.
    Mkufunzi Dotto Bulendu kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augostino cha Jijini Mwanza, akisisitiza wanahabari kuungana pamoja katika kuibua na kuandika habari/ makala zenye kutetea haki za mtoto mfanyakazi wa nyumbani
    Afisa Habari shirika la WoteSawa akizungumza kwenye mafunzo hayo
    Mwanahabari Moses Mathew kutoka gazeti Daily News akichangia mada kwenye mafunzo hayo

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI