Wakazi
wa Kata ya Itololo wilayani Kondoa Wameitaka Serikali kuwapa Faida na
Elimu Juu ya Utafiti unaotarajiwa kuanza kwenye Mapango yalipo kwenye
kijiji cha Machinjioni na kuwashirikisha wageni kutoka njee ya nchi
bila kupewa elimu wala taarifa kutoka kwa viongozi wa wizara ya
maliasili na utalii aua ofisi ya Mkuu wa wilaya.
Akizungumza
na wanahabari walitembelea kijijini Hapa Diwani Mstaafu Yahaya Giriki
alisema kuwa zoezi la utafutaji wa malikale katika eneo hilo
haujawashirikisha wananchi kwa kupewa elimu juu ya utafiti huo.
Amesema
kuwa suala hilo wao wameona wageni kutoka mataifa ya nje kufika na
kuanza kuongea na wananchi na serikali ya kijiji na wageni kuahidi
kuchangia ujenzi wa shule bila kuwashirikisha viongozi kutoka ngazi za
juu ikiwemo ngazi ya wilaya na kufika nao kwetu kututambulisha.
“Unajua
Ndugu wanahabari Suala hili linatatiza sana hatujui faida ya utafiti
huu na nini kinakuja kuvumbiliwa hapa tunaona mahema yamejengwa na
wanasema kuna watu kutoka wizarani wamekuja nao lakini hapo awali
walikuja wao kama wao bila hata mtu kutoka wizarani tutaamini vipi”
alisema Giriki.
Nae
Mmoja wa wajumbe wa serikali ya kijiji hicho anasema kuwa wanatambua
wageni hao kufika kijijini kwao miezi kadhaa iliyopita na kuzungumza na
wajumbe wa kijiji na baadae kuongea na wananchi na kukubaliana kuwa
wanakuja kuvumbua mifupa na mabaki ya dhana za kale kwenye eneo lililopo
na kujulikana kama Kisese ii.
Amesema
kuwa waliafiki jambo hilo kwa faida ya wananchi na waliomba kupatiwa
msaada wa ujenzi wa shule ya msingi ambayo imejengwa kwa nguvu za
wananchi upauzi wa paa na umaliziaji wa madarasa mawili na wageni hao
kukubali nakuanza ujenzi huo kama mnavyoona na wao wamefika hapa teyari
kuanza utafiti wao.
Suala
la wageni kutoka nje ya nchi kwenda kufanya utafiti kwenye kijiji hicho
cha Machinjiono limegubikwa na sintofahamu hadi mda huu kutowepo na
barua yeyote kutoka eneo lolote ndani ya wilaya kwenda kwenye uongozi wa
kijiji hicho licha ya kuonekana kwa mahema juhudi za kumpata kiongozi
wa watafiti hao aliyetambuliwa kwa jina moja la Catherine Raia kutoka
nje anayesoma chuo kikuu cha Dar es salaam.
Hata
hivyo juhudi zinaendelea kumtafuta Katibu mkuu wa wizara ya maliasili
na utalii au Mkurugenzi wa malikale waweze kuelezea kama wanalijua suala
hilo na hatua gani zimechukuliwa kuwapa taarifa wananchi kuhusu kadhia
hiyo au suala hili lipo kinyume na sheria.
No comments:
Post a Comment