• Breaking News

    ..

    ..

    Monday 27 November 2017

    Heche amjia juu anayemshauri Nassari

    Mbunge wa Tarime Vijijini John Heche amewachana wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi kwa kuwaambia kwamba wataendelea kuwapata wafuasi wachumia tumbo na kwamba yeye na wengine wameamua kuchagua upande wa ukweli.
    Heche amefunguka hayo baada ya kijana anayedhaniwa kuwa mfuasi wa CCM kumshauri Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kama anataka kujiendeleza Kisiasa.
    Baada ya ujumbe huo Heche imemlazimu kusema kwamba "Hizi ndio akili za kijinga za ccm kufikiri kila alieamua kuingia kwenye siasa anatafutia tumbo lake au utukufu binafsi wengine tanajua kwamba CCM ipo lakini tumechagua upande wa ukweli pamoja na maumivu tunayoyapata tutavuka na tutafika ng'ambo".

    Jibu la Heche kwa aliyekuwa akimshauri Nassari kuhama chama
    Ameongeza kwamba "Wachache wachumia tumbo mtawapata. Watu wenye moyo mwepesi ndio mnaamini hivyo jiulize wale waliopambana na wakoloni wangekua na fikra hizo leo tungekua huru?

    Ujumbe wa Nassari uliopelekea Mshauri huyo kujitokeza

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI