Na Stahmil Mohamed.
Mashindano hayo yanatarajia kushirikisha timu 11 kutoka
vilabu vya shule za sekondari za Iyunga kutoka mkoani Mbeya,Sanya juu
kutoka Kilimanjaro,Songea Boys na Londoni kutoka Mkoani
Ruvuma,Mchanganyiko wa sekondari kutoka mkoani Ruvuma mchanganyuko wa
sekondari kutoka mkoani mwanza,Mwanakwerekwe C kutoka
Zanzibar,Kibasila,Juhudi ya mkoani Dodoma pamoja na wenyeji Azania
kutoka Mkoani Dar es salaam.
Aidha kutakuwa kuwa na timu mbili za Tigers kutoka ilala na
Giants ya Temeke ambazo zinaundwa na wachezaji ambao hawapo katika
vilabu vya sekondari vilabu hivi vilianzishwa na wahitimu wa sekondari
na ambao chama hakikutaka kuona vipaji vilivyoibuliwa vinapotea bila
kulelewa katika mfumo ulio rasmi.
Hata hivyo mashindano hayo yamepewa jina la5th Tanzania
koshien National Baseball Championship yanatarajiwa kufunguliwa rasmi na
Naibu waziri wa habari na utamaduni mhe Juliana Shonza siku ya tarehe 1
Dec 2017 asubuhi.
Vile vile wataalamu wa mchezo huo kutoja nchini japan
wakishikiana na wataalamu wa hapa nchini kusimamia katika uamuzi na
sehemu ya ufundi na baada ya mashindano hayo uteuzi wa timu ya taifa ya
mchezo huo chini ya umri wa miaka 23 ambayo itashiriki mashindano ya
Afrika Mashariki yanayotarajiwa kufanyika mkoani mwanza na kushirikisha
timu kutoka kenya,Uganda kuanzia tarehe 7 Disemba2017.
No comments:
Post a Comment