• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday 29 November 2017

    WACHEZAJI WA WATAU WA YANGA WAONGEZWA KIKOSI CHA KILIMANJARO STARS

    Kocha Mkuu wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Bara, ‘Kilimanjaro Stars’, Ammy Conrad Ninje, ameongeza nyota watatu katika kikosi chake mara baada ya Baraza la Soka la Afrika Mashariki (CECAFA), kuridhia kuongezwa wachezaji watatu kwa kila timu.

    Awali, CECAFA ilihitaji wachezaji 20 tu, lakini sasa wameongeza watatu na kufanya idadi mpya ya wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ya Chalenji kwa mwaka huu kuwa 23.

    Wachezaji walioongezwa na Kipa Ramadhani Kabwili kutoka Young Africans ya Dar es Salaam, Amani Kiata  wa Nakuru All Stars ya Kenya na Yahya Zayd kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.

    Kikosi cha wachezaji 20 wa awali wa Ninje - Kocha wa Daraja ‘A’ la Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA), ni makipa Aishi Manula (Simba SC) na Peter Manyika (Singida United).

    Walinzi ni Gadiel Michael (Young Africans), Boniphace Maganga (Mbao FC), Kelvin Yondani (Young Africans), Kennedy Juma (Singida United), Erasto Nyoni (Simba SC) na Mohammed Hussein (Simba SC).

    Viungo wa kati ni Himid Mao ambaye ni Nahodha (Azam FC), Jonas Mkude (Simba SC), Hamis Abdallah (Sony Sugar/Kenya), Mzamiru Yassin (Simba SC), Raphael Daud (Young Africans), Shizza Kichuya (Simba SC), Abdul Hilal (Tusker/Kenya) na Ibrahim Ajib (Young Africans).

    Washambuliaji ni Mbaraka Yussuph (Azam FC), Elias Maguri (Dhofar/Mascat, Oman), Daniel Lyanga (Fanja FC/Mascat) na Yohana Mkomola (Ngorongoro Heroes). 

    Benchi la Ufundi linaundwa na yeye Ninje ambaye ni Kocha Mkuu, Fulgence Novatus (Kocha Msaidizi), Patrick Mwangata (Kocha wa Makipa), Danny Msangi (Meneja), Dkt. Richard Yomba (Daktari wa timu), Dkt. Gilbert Kigadye (Daktari wa Viungo) na Ally Ruvu (Mtunza Vifaa).

    Katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Desemba 3, mwaka huu, Kilimanjaro Stars imepangwa Kundi ‘A’ pamoja wenyeji Kenya, Rwanda na Libya ambayo ni timu mwalikwa kutoka Kaskazini mwa Afrika.

    Kilimanjaro Stars ambayo imewahi kutwaa mara tatu taji hilo la Chalenji tangu kuanzishwa kwake, itaaza kampeni za kurudisha heshima yake dhidi ya Libya katika kundi hilo la A utaofanyika Desemba 3, mwaka huu.

    Mashindano ya mwaka huu CECAFA ilifikia makubaliano na kanda mbili za Kusini mwa Afrika - COSAFA na ile ya Kaskazini UNAF kualika timu mbili za kutoka kanda hizo na mataifa ya Libya na Zimbabwe.

    Jumla ya timu shiriki kwenye CECAFA Senior Challenge Cup mwaka huu itakuwa 10 ambazo ni pamoja na wenyeji Kenya, Uganda, Tanzania, Rwanda, Burundi, South Sudan, Ethiopia, Zanzibar, Somalia, Zimbabwe na Libya. 

    Sudan wenyewe wamejiondoa katika mashindano ya mwaka huu wakati mataifa mawili ya Eritrea na Djibouti nayo hayatashiriki.

    Michuano hiyo itatumia viwanja vya Moi kilichopo Kisumu (Moi Stadium), Bukungu kilichopo Kakamega na Afraha kilichopo Nakuru wakati Uwanja wa Kasarani Nairobi na ule wa Kenyatta uliopo Machakos vitatumika kama viwanja vya ziada.

    Makundi 2017 Cecafa Challenge Cup
    Kundi A: Kenya, Libya, Rwanda, Tanzania, Zanzibar.
    Kundi B: Uganda, Zimbabwe, Burundi, Ethiopia, South Sudan.

    Ratiba ya michuano hiyo mwaka huu ni kama ifuatavyo:
    Desemba 3, 2017
    Kundi A
    Libya vs Tanzania
    Kenya vs Rwanda

    Desemba 4, 2017
    Kundi B
    Burundi vs Ethiopia
    Uganda vs Zimbabwe
    Desemba 5, 2017
    Kundi A
    Zanzibar vs Rwanda
    Kenya vs Libya
    Desemba 6, 2017
    Kundi B
    Sudan Kusini vs Zimbabwe
    Uganda vs Burundi

    Desemba 7, 2017
    Tanzania vs Zanzibar
    Rwanda vs Libya

    Desemba 8, 2017
    Kundi B
    Sudan Kusini vs Ethiopia
    Zimbabwe vs Burundi

    Desemba 9, 2017
    Kundi A
    Rwanda vs Tanzania
    Kenya vs Zanzibar
    Desemba 10, 2017
    Kundi B

    Sudan Kusini vs Burundi
    Ethiopia vs Uganda

    Desemba 11, 2017
    Kundi A
    Libya vs Zanzibar
    Kenya vs Tanzania

    Desemba 12, 2017
    Kundi B
    Uganda vs Sudan Kusini
    Zimbabwe vs Ethiopia

    Desemba 13, 2017
    Mapumziko
    Desemba 14, 2017
    Nusu fainali 1 (Mshindi Kundi A vs Mshindi wa pili Kundi B)
    Desemba 15, 2017

    Nusu fainali 2 (Mshindi Kundi B vs Mshindi wa pili kundi A)
    Desemba 16, 2017

    Mapumziko
    Desemba 17, 2017
    Mshindi wa Tatu & Fainali

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI