Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Himid
Mao ‘Ninja’, amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Azam FC (NMB Player Of
The Month) mwezi Oktoba-Novemba.
Nahodha wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Himid Mao ‘Ninja’
Mao aliyeshindanishwa na wachezaji wengine wanne wa Azam FC, akiwemo
Nahodha Msaidizi, Agrey Moris, kipa Razak Abalora na beki Bruce Kangwa,
anakuwa mchezaji wa tatu msimu huu kutwaa tuzo hiyo baada ya Yakubu
Mohammed kufanya hivyo Agosti-Septemba na mshambuliaji Mbaraka Yusuph
aliyeibeba Septemba-Oktoba.
Nahodha huyo msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’,
ametwaa tuzo hiyo baada ya kujizolea kura 320 za mashabiki zikiwa ni
asilimia 47 ya kura zote 680 zilizopigwa kupitia mtandao wa poll kwenye
akaunti ya facebook ya Azam FC.
Aidha kipa mahiri wa timu hiyo, Razak Abalora, ambaye mpaka sasa
amefungwa mabao matatu kwenye mechi 11 za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara (VPL) ameshika nafasi ya pili baada ya kujizolea kura 292 sawa na
asilimia 43 za kura zote zilizopigwa.
Beki wa kushoto, Kangwa ameshika nafasi ya nne kwa kura 41
alizojizolea (asilimia sita) huku Moris akimalizia orodha hiyo baada ya
kukusanya kura 27 zikiwa ni asilimia nne za kura zote zilizopigwa na
mashabiki (680).
Tuzo hiyo inadhaminiwa na Wadhamini wakuu wa Azam FC, Benki ya NMB
No comments:
Post a Comment