• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 23 November 2017

    WATANZANIA WATAKIWA KUJITOKEZA KWENYE ONYSHOLA HISTORIA

    Na stahmili Mohamed.
    Ikiwa ni mwendelezo wa programu ya Museum Art Explosion inayofanyika kila ijumaa ya mwisho wa mwezi  iliyoandaliwa na Makumbusho ya Taifa  ikiwa na lengo La kuwaleta wasanii na kutoa fursa ya kuonesha vipaji vyao na ufundi wa majukwaa na kuuza kazi zao kwa watanzania na wageni mbalimbali Makumbusho ya Taifa ikishirikiana na kundi La wasanii la Kaleleo sanaa Network wameandaa onesho la  jukwaani la igizo LA "Fumo Liongo" ikiwa na lengo  LA kurejesha hadhi na thaman ya majukwaa.
    Hayo yamesemwa na Mkuu wa idara ya program Makumbusho ya Taifa Bw.Chance Ezekiel alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na onesho hilo kuwa litafanyika hapo kesho saa moja kamili usiku katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa na mgeni rasmi atakuwa ni Waziri wa habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe lengo ni kufufua Sanaa ambazo zinaonekana kupitwa kiteknologia.
    Hata hivyo Bw .Azekiel amesema moja ya kazi za Makumbusho ya Taifa ni kuhifadhi na kurithisha utamaduni wa mtanzania kwa vizazi vilivyopo na vijavyo wameona IPO haja ya kurithisha utamaduni wa kazi bora za sanaa za jukwaani kwa wasanii chipukizi na wapenda Sanaa kwa ujumla pia  tangu walipoanza  program ya Museum Art Explosion  kuna faida nyingi zimepatikana ikiwa in kuinua hari za wasanii kwani hupata fursa nyingi za mialiko nje ya nchi na Makumbusho hufaudika kwa kuhifadhi kumbukumbu za kazi na historia za wasanii hao hususan waluobibea katika tasnia hii.
    Kwa upande wake msanii  na muongozaji wa onyesho hilo  Bw Ghonche Materego amesema ni wakati wa kuthamini kazi za Sanaa za majukwaa  kwani zinamashiko zaidi pia amewataka wasanii ,wanafunzi wa sekondari pamoja na vyuoni watanzania kiujumla kujitokeza kwa wingi katika onyesho hilo  ambalo linaonyesha  na kuelezea historia ya MTU maarufu na shujaa aitwae Liongo aliyeishi  pwani ya Afrika Mashariki katika karne ya 15 kwa shilingi elfu kumi tu kwa mkubwa na shilingi elfu tano kwa mtoto zaidi ya yote watu wote watajifunza na kuburudika.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI