Na stahmil Mohammed
Hospitali ya taaluma ya chuo kikuu cha afya na sayansi
shirikishi muhimbili MUHAS iliyopo katika kampasi ya mloganzila,
inatalajiwa kufunguliwa rasmi siku ya jumamosi tarehe 25 mwezi huu na
mgeni rasmi atakuwa rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, John pombe
magufuli ambaye amechangia kwa kiasi kikubwa mpaka hospitali hiyo
kukamilika ambapo ujenzi ulikamilika rasmi mwezi agosti 2016.
Akiongea Leo kaimu mkuu wa chuo Prof. Appolinary Kamuhabwa
amesema kuwa hospitali hiyo inatambulika kama MUHAS academic medical
centre (MAMC) na imepewa hadhi ya hospitali ya Taifa ya rufaa yenye
uwezo wa kutoa huduma za afya zinazohitaji madaktari bingwa na madaktari
waliobobea.
Pia amesema kuwa MAMC imejengwa kwa kiwango cha hali ya juu
na cha kisasa ili iweze kutumika katika kufundisha watalaam wa huduma
za afya, kutoa huduma za uchunguzi wa magonjwa na kufanya tafiti za
afya.
Prof. kamuhabwa amesema kuwa ujenzi wa hospitali hiyo
umefanyika chini ya ufadhili wa serikali ya jamhuri ya muungano wa
Tanzania kupitia mkopo laini (soft loan) kutoka serikali ya jamhuri ya
korea.
Aidha Prof.kamuhabwa amebainisha matibabu yatakayokuwa
yanatolewa hospitalini hapo na kusema kuwa hospitali ya taaluma na tiba
ina vitanda vya kulaza wagonjwa 571, na ina vitengo vyote
vinavyohitajika katika kutoa huduma za kibingwa ambapo ametaja baadhi ya
huduma hizo kuwa ni huduma za Tiba ya dharura na ajali kwa wakubwa na
watoto, huduma za mfumo wa uzazi, huduma za upasuaji mkubwa na mdogo,
huduma za magonjwa ya akili huduma za magonjwa ya kinywa, huduma ya
magonjwa ya mifupa na majeruhi pamoja na huduma za magonjwa wa macho,
mfumo wa pua, koo na masikio.
Profesa kamuhabwa amemaliza kwa kusema mradi huo umegharimu
shilingi milioni94.5 dolla za kimarekani baada ya kupata mkopo laini
kutoka korea ya kusini ambapo imetoa dolla milioni 49.5 za kimarekani na
Tanzania imetoa dolla milioni 18.40.pia amesema hospitali hiyo imekuwa
na wauguzi wapya na waliohamishwa mikoa249,wauguzi kutoka muhimbili
229,na imetoa vibali vya kazi 259 hivyo itakuwa na wauguzi zaidi ya 807
hivyo huduma zitafanywa kwa weledi
No comments:
Post a Comment