Na Stahmil Mohamed
Kutokana na kuongezeka kwa tatizo la sumu kuvu kwenye vyakula hasa kwenye zao la mahindi ambalo takribani nchi 16 kutoka Afrika zinategemea zao hilo, umoja wa afrika kupitia programu ya udhibiti wa aflatoksini barani afrika (PACA) kwa kushirikiana na taasisi nyingine imeadaa kongamano kwa lengo la kupunguza ongezeko la aflatoksini katika vyakula.
Kutokana na kuongezeka kwa tatizo la sumu kuvu kwenye vyakula hasa kwenye zao la mahindi ambalo takribani nchi 16 kutoka Afrika zinategemea zao hilo, umoja wa afrika kupitia programu ya udhibiti wa aflatoksini barani afrika (PACA) kwa kushirikiana na taasisi nyingine imeadaa kongamano kwa lengo la kupunguza ongezeko la aflatoksini katika vyakula.
Akiongea Leo Raymond Wigenge ambaye ni mkurugenzi wa
masuala ya usalama wa chakula TFDI amesema kuwa aflatoksini inasababisha
madhara makubwa katika usalama wa chakula na pia huadhiri afya za watu
na maendeleo yao.
Pia Raymond amesema kuwa inakadiliwa kuwa watu milioni 208
katika bara la afrika wanategemea mahindi kama chakula chao kikuu ambapo
nchi 16 kati ya 22 ulimwenguni ambazo zinategemea mahindi kama chakula
chao kukuu, ziko barani afrika.
"Nchi 16 kati ya 22 ulimwenguni zinazotegemea zao la mahindi kama chakula kikuu zinatoka barani afrika" amesema Raymond.
Pia ameongeza kuwa kongamano hilo linawaunganisha kwa
pamoja watalaam kutoka vyama vya wakulima, wataalam wa kilimo, watalaam
wa afya, watalaam wa lishe pamoja na wafanya biashara ili kwa pamoja
waweze kugundua njia bora ya udhibiti wa usambaaji wa sumu kuvu kwenye
mahindi barani afrika.
"Katika kongamano hili tutakuwa na vyama mbalimbali kama
vile vyama vya wakulima, watalaam wa afya, watalaam wa kilimo, watalaam
wa lishe pamoja na wafanya biashara ili kwa pamoja waweze kugundua njia
bora ya udhibiti wa usambaaji wa sumu kuvu kwenye mahindi barani
afrika".
Pia Raymond amebainisha hasara na madhara yanayotokana na
sumu kuvu kuwa ni kansa ya maini, kudumaa kwa watoto, lakini pia amesema
kuwa bara la afrika hupoteza milioni 600 za kimarekani kwa mwaka kwa
kutupa mahindi yaliyochafuliwa na sumu kuvu.
"Afrika hupoteza milioni 600 za kimarekani kwa kutupa
mahindi yaliyochafuliwa na sumu kuvu lakini pia sumu kuvu husababisha
Kansa ya maini na kudumaa kwa watoto" amebainisha Raymond.
No comments:
Post a Comment