Azam FC kwasasa ina alama 23 sawa na Simba yenye alama 23 zikitofautiana idadi ya mbao ya kufunga na kufungwa. Endapo Azam FC itashinda leo itafikisha alama 26 na kuongoza ligi huku ikisubiri matokeo ya mechi ya kesho kati ya Ndanda FC na Simba.
Baada ya mchezo wa leo mabingwa hao watetezi wa Kombe la Mapinduzi watasafiri kuelekea Visiwani Zanzibar kwaajili ya michuano ya kombe hilo inayotarajiwa kuanza Januari mwakani. Azam FC ilitwaa kombe hilo Januari mwaka huu kwa kuifunga Simba kwenye mchezo wa fainali.
No comments:
Post a Comment