Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemtaka Meneja wa TANESCO wilaya ya
Ruangwa, Bw. Samuel Pyuza kuhakisha umeme unapatikana mapema kwenye
pampu ya maji ili kukamilisha mradi wa maji wa Namahema ‘A’.
Hadi kukamilika kwake mradi huo utagharimu Sh. milioni 244.52, na utahudumia wakazi 2,257 wa vijiji hivyo viwili ambao walikuwa wanasongamana kupata maji kutoka kwenye kisima ambacho kilikuwa kinatumia pampu ya mkono.
Waziri Mkuu yuko kwenye mapumziko ya mwisho wa mwaka, lakini ameanza ziara fupi ya siku tatu, kukagua miradi ya maendeleo jimboni kwake katika wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.
Jumla ya sh. milioni 189.93 zimeshatumika kwenye mradi huo ambazo ni sawa na asilimia 77.68 ya fedha ziliopangwa kutumika. Kijiji cha Namahema ‘A’ kina watu 1,668 na Namahema ‘B’ kina watu 589
No comments:
Post a Comment