Mkuu wa Jeshi la polisi nchini Tanzania (IGP) Simoni Sirro,
amewahakikishia Watanzania wote kuwa wameimarisha ulinzi na usalama
katika kipindi hiki cha sikukuu.
IGP
Sirro amesema hayo Mkoani Lindi alipokuwa katika ziara ya kikazi
nakuwataka watanzania washerehekee sikuuu za Krismas na Mwaka mpya kwa
uhuru, kwani wao kama jeshi la polisi wamejipanga kwa ulinzi wa raia na
mali zao.
"Timu zetu mbalimbali zimejipanga tumeanza doria tayari kabisa kwa kuimarisha ulinzi na usalama kwa raia wema na pia natoa tahadhari kwa wale watu ambao wanafikiria kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani hatua kali za kisheria tutachukua dhidi yao.
IGP Sirro anasema hayo zikiwa zimebakia siku chache tu kuelekea kwenye sikukuu hizo za mwisho wa mwaka.
"Timu zetu mbalimbali zimejipanga tumeanza doria tayari kabisa kwa kuimarisha ulinzi na usalama kwa raia wema na pia natoa tahadhari kwa wale watu ambao wanafikiria kufanya vitendo vya uvunjifu wa amani hatua kali za kisheria tutachukua dhidi yao.
IGP Sirro anasema hayo zikiwa zimebakia siku chache tu kuelekea kwenye sikukuu hizo za mwisho wa mwaka.
No comments:
Post a Comment