• Breaking News

    ..

    ..

    Friday 22 December 2017

    Vijana watakiwa kuacha kujihusisha na siasa na badala yake kuwa wazalendo.



    Na Stahmili Mohammed.

    Jumuiya ya Chuo kikuu cha Dar es salaam (DARUSO)imewataka Vijana kuacha kuwa wafia siasa na kuwa wazalendo ili kulisaidia Taifa lizidi kukua kiuchumi hasa katika Kipindi hiki ambacho nchi inaelekea katika uchumi wa Viwanda.

    Haya yamezungumzwa na Rais wa Chuo kikuu cha  Dar es salaam Jeremiah John Jilili alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kumekuwa na dhana kwa vijana ya kulowea kwenye siasa na kulalamika pasipokufanya utafiti  hali ambayo inalirudisha nyuma Taifa ambalo kwa Sasa linaelekea katika uchumi wa kati wa Viwanda hivyo waachane na dhana ya malalamiko.

    Aidha Jilili amesema kupitia mijadala ,midahalo mbalimbali amegundua na kujiridhisha kuwa vijana wengi wa kitanzania wanauelewa mkubwa mpana na takwimu sahihi za masuala ya nchi yetu lakini wanayumbishwa na mambo ya kiitikadi kitu ambacho tukiwa wazalendo hayana tija kwenye Taifa letu.

    Pia Jilili amewahasa vijana kubadilika  na  kusema kuwa  vijana ndio chachu kubwa ya mabadiliko na maendeleo kwenye nchi yoyote ile duniani.

    "Vijana tunatakiwa tubadilike kwani vijana ndio chachu ya maendeleo kwenye nchi yoyote ile duniani" amesema Jilili.

     Sambamba na hayo Jilili amempongeza Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuri kwa kuwa mzalendo na kuendelea kusimamia matumizi mazuri  ya rasilimali za nchi.

    "Tunampongeza Rais kwa kuwa mzalendo na kuendelea kudhibiti matumizi mabaya ya rasilimali za nchi"amesema Jilili.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI