Na Stahmil Mohamed
.
.
Hayo yamesemwa na Daktari wa chuo kikuu cha sayansi na tiba
muhimbili professa Karim Manji alipokuwa akizungumza katika warsha ya
fikrafya iliyofanyika Leo lengo likiwa ni kutoa mafunzo kuhusiana na
matatizo ya afya ya Akili na jinsi ya kukabiliana na tatizo hilo ambapo
amesema kuna haja ya kujitaarisha kifkra ili kuepukana na maradhi ya
moyo yanayotokana na mawazo yakupiliza pamoja na matatizo ya Akili na
kuwataka watanzania wachukulie changamoto mbalimbali wanazozipata ni za
mda na zipo hivyo wasikate tamaa na kujikataa moja kwa moja kwakujiona
hawafai katika jamii jambo ambalo sio la kweli na ni hatari kwa afya ya
Akili pamoja na mwili.
Professa Manji ameendelea kwa kueleza kuwa japo si rahisi
binadamu kukosa mawazo ila amewataka wasipitilize kufikiria kwakuwa
athari zake ni kubwa kwa afya ya akili na moyo na ndio maana wameamua
kukutana kujadili na kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali wakiwemo
walimu,wanasheria,manesi pamoja na madaktari ili kupata matokeo chanya
kwenye jamii ili kukabiliana na tatizo hili
Naye Mwenyekiti wa Fikrafya Dkt Shabil Hussein amesema
wameamua kuielimisha jamii kuhusiana na matatizo ya ubongo na Akili
kwenye jamii kwa kuwa ni tatizo ambalo jamii wanalichukulia kwa mtazamo
tofauti kuwa kila mwenye tatizo la akili ni lazima awe na muonekano
ambao haufanani na watu wengine Bali kuna aina nyingi ya magonjwa ya
Akili kwani kunabaadhi ya watu wapo maofisini wanakabiliwa na matatizo
ya Akili yanayotokana na mawazo yaliyopitiliza(stress)kutokana na
changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo kila siku hivo wanajipanga
kutoa elimu nchi nzima kuhusiana na matatizo ya afya ya Akili na namna
ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazosababisha
Pia Daktari bingwa wa afya ya akili Dkt Saidi Kuganda
amesema kupitia warsha ya Leo ya mafunzo maalumu ya kwa wadau mbalimbali
ameona jamii itafaidika kupitia mafunzo hayo pia jamii itaelimika
kuhusiana na afya ya elimu ameendelea kwa kusema kuwa takwimu
inayotolewa kuwa kila watu 4 mmoja anawezekana akawa na matatizo ya afya
ya akili hiyo haimaanishi kuwa ni wameathirika zaidi hivyo elimu
itakayotolewa kuhusiana na afya ya akili kupitia fikrafya itakuwa
chachu ya kuelimika katika jamii.
No comments:
Post a Comment