• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday 27 January 2018

    Lowassa Amrushia madongo Mtulia



    Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa amefunguka na kuwataka wanachama na viongozi wa CHADEMA kuacha kumtaja taja mgombea Ubunge wa CCM Kinondoni Maulid Mtulia kwani mtu huyo ni wa hovyo hastaili kutajwa tajwa kwani kufanya hivyo ni kumpa kichwa. 
    Lowassa amesema hayo leo Januari 27, 2018 akiwa katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa marudio katika jimbo la Kinondoni ambapo leo maelfu ya wananchi wa Kinondoni wameweza kuwasikiliza viongozi mbalimbali wa CHADEMA kwa hoja na sera mbalimbali kuelekea uchaguzi huo ambao unatarajiwa kufanyika Februari 17, 2018.
    "Kwanza nawashauri huyu Mtulia msimseme seme sana wanini huyu, mtu hovyo kabisa huyu mnampa kichwa tu sasa mtu hovyo hapaswi kuchukua muda wenu kumjadili bali nachotaka tushughulike kuwaelimisha wananchi wa Kinondoni kwanini wanastahili kutupa sisi kura, habari ya huyu bwana tuachane naye, hawa CCM hawaeleweki kule Moshi na Korogwe tulishinda lakini wakaja kusema tumeshindwa hivyo nataka kusema saizi tujiandae kulinda kura zetu" alisema Lowassa
    Mbali na hilo Lowassa alimnadi Salum Mwalimu kwa kusema kuwa ni kijana safi ambaye anastahili kwenda Bungeni kuwasemea wananchi wa Kinondoni

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI