Msanii mkongwe wa filamu za bongo, Mzee Majuto amefunguka na kudai yeye
ndio mtu wa kwanza kutabiri ujio wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi
ya Tanzania huku akisisitiza kwamba anajisikia faraja kuona ana misimamo
iliyokuwa imara.
"Mimi ndiyo mtu wa kwanza kumtabiri kwamba akiwa Rais itakuwa shughuli. Nilishukuru sana kuchaguliwa huyu bwana, tumepata Rais sio masihara watu wote sasa hivi wana adabu zao wanajua nini maana ya kazi ukisema jambo watu wanatekeleza, wezi wanakamatwa, wala rushwa wanakamatwa, wenye vyeti feki hata kama amefanya kazi miaka 20 fukuza, hii safi", alisema Majuto.
Pamoja na hayo, Mzee Majuto aliendelea kwa kusema "sisi wazee tunafarijika sasa hivi, viwanda kila kona vimetapakaa na leo amekuja kutembea hospitalini hapa sijui kama wengine hawajikojolea huko kwa uoga maana hataki masihara. Hii ndio raha ya kupata viongozi wenye msimamo".
Kwa upande mwingine, Mzee Majuto amesema kupata sio rahisi kupata Rais mwenye misimamo na asiyekuwa na masihara kama Dkt. John Magufuli.
No comments:
Post a Comment