• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday 31 January 2018

    "Nilimtabiria Rais Magufuli"- Majuto

    Msanii mkongwe wa filamu za bongo, Mzee Majuto amefunguka na kudai yeye ndio mtu wa kwanza kutabiri ujio wa Rais Magufuli katika kuongoza nchi ya Tanzania huku akisisitiza kwamba anajisikia faraja kuona ana misimamo iliyokuwa imara.
    Mzee Majuto amebainisha hayo muda mchache alipotembelewa na Rais Magufuli leo katika hospitali aliyolazwa ya  ya Tumaini iliyopo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa tezi dume unaomsumbua kwa kipindi kirefu.
    "Mimi ndiyo mtu wa kwanza kumtabiri kwamba akiwa Rais itakuwa shughuli. Nilishukuru sana kuchaguliwa huyu bwana, tumepata Rais sio masihara watu wote sasa hivi wana adabu zao wanajua nini maana ya kazi ukisema jambo watu wanatekeleza, wezi wanakamatwa, wala rushwa wanakamatwa, wenye vyeti feki hata kama amefanya kazi miaka 20 fukuza, hii safi", alisema Majuto.
    Pamoja na hayo, Mzee Majuto aliendelea kwa kusema "sisi wazee tunafarijika sasa hivi, viwanda kila kona vimetapakaa na leo amekuja kutembea hospitalini hapa sijui kama wengine hawajikojolea huko kwa uoga maana hataki masihara. Hii ndio raha ya kupata viongozi wenye msimamo".
    Kwa upande mwingine, Mzee Majuto amesema kupata sio rahisi kupata Rais mwenye misimamo na asiyekuwa na masihara kama Dkt. John Magufuli.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI