Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
ameahidi kutoa pesa za kitanzania jumla ya Bilioni 10 Kwa Idara ya
Uamiaji nchini ili kuboresha makao makuu ya idara hiyo.
Akizungumza
leo katika uzinduzi wa Pasi za kusafiria za mfumo wa kielektroniki,
Rais Magufuli amesema kwamba ameamua kutoa pesa hizo kutokana na
uzalendo unaooneshwa na Idara hiyo.
Rais Magufuli amesema kuwa kutokana na jinsi idara hiyo inavyojitahidi kufanya kazi kwa juhudi kubwa ndiyo maana aliamua kuwapatia nyumba 103 mkoani Dodoma ambapo serikali imewahamishia makazi yake na kuongeza kuwa ni taasisi ya kwanza kupatiwa nyumba katika mji huo.
"Dkt. Makakala Katafute eneo, nitawapa bilioni 10 wakati wowote mutakapozihitaji muanze kujenga makao makuu ya uhamiaji, na natoa hizi kwa shukrani ya kazi nzuri unayofanya wewe na watendaji wako". Rais Magufuli
Ameongeza "Hapa jinsi palivyokaa kaa hapafananii na makao makuu ya uhamiaji. Na kwa vile mmekubali kuhamia Dodoma ni lazima tuwe na jengo zuri litakalokaa kama makao makuu ya Immigration yenye 'parking nzuri hata mtu akitoka huko anajua kwamba anakwenda uhamiaji. Najua kuna baadhi ya wafanyakazi watalaumu kuhama kwa sababu wanajua wanachofanyaga kwenye yale mabanda yale na mbinu zao za kutengeneza michuzi".
Rais Magufuli amesema kuwa kutokana na jinsi idara hiyo inavyojitahidi kufanya kazi kwa juhudi kubwa ndiyo maana aliamua kuwapatia nyumba 103 mkoani Dodoma ambapo serikali imewahamishia makazi yake na kuongeza kuwa ni taasisi ya kwanza kupatiwa nyumba katika mji huo.
"Dkt. Makakala Katafute eneo, nitawapa bilioni 10 wakati wowote mutakapozihitaji muanze kujenga makao makuu ya uhamiaji, na natoa hizi kwa shukrani ya kazi nzuri unayofanya wewe na watendaji wako". Rais Magufuli
Ameongeza "Hapa jinsi palivyokaa kaa hapafananii na makao makuu ya uhamiaji. Na kwa vile mmekubali kuhamia Dodoma ni lazima tuwe na jengo zuri litakalokaa kama makao makuu ya Immigration yenye 'parking nzuri hata mtu akitoka huko anajua kwamba anakwenda uhamiaji. Najua kuna baadhi ya wafanyakazi watalaumu kuhama kwa sababu wanajua wanachofanyaga kwenye yale mabanda yale na mbinu zao za kutengeneza michuzi".
No comments:
Post a Comment