Winga wa Ujerumani Mesut Ozil amesaini mkataba mpya wa miaka mitatu na nusu kuendelea kubaki Arsenal mpaka mwezi Juni 2021.
Leo ni siku nzuri kwa Arsenal ikiwa imetoka kukamilisha usajili wa Pierre Aubameyang kutoka Borrusia Dortmund. Mkataba wa awali wa ozil ulikuwa unamalizika mwezi juni mwishoni wa msimu huu.
Ozil mwenye miaka 29 alijiunga na washika mitutu hao wa jiji la London mwaka 2013 akitokea klabu ya Real Madrid kwa dau la rekodi ya klabu £ 42.4m (Bilioni 119) ambayo leo imevunjwa na usajili wa Aubameyang kwa dau la £ 56 (Bilioni 156).
No comments:
Post a Comment