Mke wa Mzee Majuto ambaye anafahamika kwa jina la Aisha Mbwana
amefunguka na kuwaomba Watanzania waendelee kumuombe Mzee Majuto ili
aweze kupona maradhi ambayo yanamsumbua na kusema sasa hivi mumewe
amelazwa katika hospitali ya Tumaini.
Akiongea
na moja ya chombo cha habari nchini Aisha amesema kuwa toka jana majira
ya saa kumi jioni alipokwenda kwenye hospitali hiyo ya Tumaini
walilazwa kutokana na mume wake kusumbuliwa na tatizo la tezi dume
ambalo limeanza kumsumbua takribani miezi miwili sasa.
"Tumekuja hospitali kuanzia jana saa kumi jioni na tumelazwa kwani Mzee Majuto anaumwa anasumbuliwa na tatizo la tezi japo kuwa hayupo 'serious' sana kama ambavyo watu wanafikiria, napenda kuwaambia Watanzania na mashabiki wa Mzee wazidi kumuombea Mungu kwa sababu bado tunamuhitaji", amisema Aisha Mbwana
Kwa upande wake Mzee Majuto akiwa hospitali hapo ambapo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji aliweza kuongea na kusema kuwa yeye anazidi kupambana kuhakikisha anatibu ugonjwa huo na kudai kuwa kuugua ni ibada.
"Tumekuja hospitali kuanzia jana saa kumi jioni na tumelazwa kwani Mzee Majuto anaumwa anasumbuliwa na tatizo la tezi japo kuwa hayupo 'serious' sana kama ambavyo watu wanafikiria, napenda kuwaambia Watanzania na mashabiki wa Mzee wazidi kumuombea Mungu kwa sababu bado tunamuhitaji", amisema Aisha Mbwana
Kwa upande wake Mzee Majuto akiwa hospitali hapo ambapo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji aliweza kuongea na kusema kuwa yeye anazidi kupambana kuhakikisha anatibu ugonjwa huo na kudai kuwa kuugua ni ibada.
No comments:
Post a Comment